Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dk. Adelardus Kilangi akitoa mada kuhusu Nafasi na Majukumu ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wakati wa mkutano unaoendelea wa Mawakili wa Serikali waliokatika utumishi wa umma. Pamoja na mambo mengine Dk. Kilangi amesema Mawakili wa Seriakali walio katika utumishi wa umma watakuwa na chama chao.
Sehemu ya mawakili wa serikali kutoka wizara mbalimbali, Idara na Taasisi zinazojitegema, Wakala na Serikali za Mitaa ambao wapo Jijini Dodoma kwa mkutano wao wa siku mbili.
Na Mwandishi Maalum, Dodoma
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dk. Adelardus Kilangi amesema, anakusudia
kuanzisha Chama cha Wanasheria walio katika utumishi wa Umma.
Dk. Kilangi ameyaeleza hayo wakati akiwasilisha mada kuhusu Nafasi na
Majukumu ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa Mawakili wa
Serikali walio katika utumishi wa umma wanaokutana katika mkutano wao wa
siku mbili unaofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Mipango
Jijini Dodoma.
Mawakili hao wa Serikali wapatao mia tisa ( 900) wanatoka Wizara
mbalimbali, Idara za Serikali, Taasisi na Mashirika yanayojitegemea, Wakala
na Mamlaka za Serikali za Mitaa. Mkutano huo ambao ni wa pili kufanyikia
ulifunguliwa na Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali amebainisha kwamba, kuanzishwa kwa Chama
hicho ni kwa mujibu wa Ibara ya 74 ya Muswaada wa Sheria ya Marekebisho
Mbalimbali ( Na.2) 2018 inayoeleza kuwa , “ Mwanasheria Mkuu wa Serikali
anaweza kuanzisha Chama cha Wanasheri katika Utumishi wa Umma”.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...