Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dk. Adelardus Kilangi akitoa mada kuhusu Nafasi na Majukumu ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wakati wa mkutano unaoendelea wa Mawakili wa Serikali waliokatika utumishi wa umma. Pamoja na mambo mengine Dk. Kilangi amesema Mawakili wa Seriakali walio katika utumishi wa umma watakuwa na chama chao.
Sehemu ya mawakili wa serikali kutoka wizara mbalimbali, Idara na Taasisi zinazojitegema, Wakala na Serikali za Mitaa ambao wapo Jijini Dodoma kwa mkutano wao wa siku mbili.

Na Mwandishi Maalum, Dodoma

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dk. Adelardus Kilangi amesema, anakusudia kuanzisha Chama cha Wanasheria walio katika utumishi wa Umma. Dk. Kilangi ameyaeleza hayo wakati akiwasilisha mada kuhusu Nafasi na Majukumu ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa Mawakili wa Serikali walio katika utumishi wa umma wanaokutana katika mkutano wao wa siku mbili unaofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Mipango Jijini Dodoma.

Mawakili hao wa Serikali wapatao mia tisa ( 900) wanatoka Wizara mbalimbali, Idara za Serikali, Taasisi na Mashirika yanayojitegemea, Wakala na Mamlaka za Serikali za Mitaa. Mkutano huo ambao ni wa pili kufanyikia ulifunguliwa na Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali amebainisha kwamba, kuanzishwa kwa Chama hicho ni kwa mujibu wa Ibara ya 74 ya Muswaada wa Sheria ya Marekebisho Mbalimbali ( Na.2) 2018 inayoeleza kuwa , “ Mwanasheria Mkuu wa Serikali anaweza kuanzisha Chama cha Wanasheri katika Utumishi wa Umma”.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...