Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amemuagiza Mkuu wa wilaya ya Sumbawanga, Dk. Halfan Haule kutumia mamlaka yake kuwatupa ndani saa 48 wasimamizi wa utekelezaji wa mradi wa usambazaji umeme vijijini (REA) awamu ya tatu wa Kampuni ya Nakuroi Investment iwapo watasuasua katika ujenzi wa miundombinu ya umeme wilayani humo.
Naibu Waziri huyo, ametoa agizo hilo leo akiwa katika kijiji cha Kilyamatundu kilichopo mpakani mwa mikoa ya Mbeya na Songwe tarafa ya Kipeta wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi inayolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya REA awamu ya tatu mkoani humo.
Kabla ya kutoa agizo hilo, Naibu Waziri huyo alionyeshwa miundombinu inayowezesha upatikanaji wa umeme katika kijiji jirani cha Kamsamba iliyopo umbali wa mita 100 na kuonyesha kushangazwa kwanini Kijiji cha Kilyamatundu kinashindwa kunufaika na huduma ya umeme kwa kuwa miundombinu ipo jirani kiasi hicho.
"Mkandarasi nataka nguzo na vifaa vingine vifike hapa Alhamisi ijayo kama ulivyoahadi na ujenzi wa miundombinu ya umeme ianze mara moja,mkuu wa wilaya hakikisha inatumia mamlaka yako kuwatupa ndani saa 48 hawa jamaa kama watasuasua kutekeleza mradi huu, sisi lengo letu umeme upatikane hapa kijijini haraka iwezekanavyo" alisema
Baadhi ya watumishi wa Shirika la umeme nchini, Tanesco mkoawa Rukwa wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri Subira Mgalu wakati aliwahutubia wananchi wa kata ya Mtowisa mkoani Rukwa leo, ambapo yupo katika ziara ya kikazi ya kukaguautekelezaji wa miradi ya REA awamu ya tatu.(0150).


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...