Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Uganda, Balozi Patrick Mugoya
akisoma hotuba ya ufunguzi ya Mkutano wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya
Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Uganda unaofanyika jijini Kampala
kuanzia tarehe 21 hadi 23 Agosti 2018. Balozi Mugoya katika hotuba yake
alisisitiza umuhimu wa Tanzania na Uganda kuboresha miundombinu na
kuondoa vikwazo vya kibiashara ili kupunguza gharama za kufanya biashara
kati ya Tanzania na Uganda
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Salvator Mbilinyi ambaye pia ni kiongozi wa ujumbe wa Tanzania katika ngazi ya maafisa waandamizi akisoma hotuba katika ufunguzi wa mkutano wa JPC. Bw. Mbilinyi alisema kuwa Mkutano huo pamoja na mambo mengine utathimni utekelezaji wa masuala yaliyokubalika wakati wa mkutano wa kwanza wa JPC uliofanyika Arusha mwezi Aprili 2017 na kuweka mikakati ya utekelezaji kwa masuala ambayo hayajakamilika.
Balozi Mugoya na Bw. Mbilinyi wakiwa katika meza kuu kabla hawajasoma hotuba za ufunguzi.
Kutoka kushoto ni Bw. Mbilinyi, Bw. Innocent Luoga, Kamishna wa Nishati kutoka Wizara ya Nishati na Bi. Tuma Abdallah Kaimu Mhariri Mtendaji wa kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN) wakiwa katika meza kuu.
Sehemu ya Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia hotuba za ufunguzi wa Mkutano wa JPC. Kutoka kushoto ni Bi. Mwadawa Ali kutoka kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN), Bw. Paul Makelele kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Bw. Karim Msemo wa Wizara ya Mifugo.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Salvator Mbilinyi ambaye pia ni kiongozi wa ujumbe wa Tanzania katika ngazi ya maafisa waandamizi akisoma hotuba katika ufunguzi wa mkutano wa JPC. Bw. Mbilinyi alisema kuwa Mkutano huo pamoja na mambo mengine utathimni utekelezaji wa masuala yaliyokubalika wakati wa mkutano wa kwanza wa JPC uliofanyika Arusha mwezi Aprili 2017 na kuweka mikakati ya utekelezaji kwa masuala ambayo hayajakamilika.
Balozi Mugoya na Bw. Mbilinyi wakiwa katika meza kuu kabla hawajasoma hotuba za ufunguzi.
Kutoka kushoto ni Bw. Mbilinyi, Bw. Innocent Luoga, Kamishna wa Nishati kutoka Wizara ya Nishati na Bi. Tuma Abdallah Kaimu Mhariri Mtendaji wa kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN) wakiwa katika meza kuu.
Sehemu ya Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia hotuba za ufunguzi wa Mkutano wa JPC. Kutoka kushoto ni Bi. Mwadawa Ali kutoka kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN), Bw. Paul Makelele kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Bw. Karim Msemo wa Wizara ya Mifugo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...