Na Woinde Shizza,Arusha .

 Mkuu mpya wa wilaya ya Arumeru Mhe. Jerry Muro amewaahidi  watumishi wa halmashauri ya Meru kuwapa ushirikiano wa kuweza kutimiza majukumu yao ikiwa ni njia mojawapo ya kutoa  huduma bora kwa wananchi . 

 Hayo aliyasema wakati alipokuwa akizungumza na wafanyakazi, watumishi wa halmashauri hiyo katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo ambapo aliwahaidi kuwapa ushirikiano watumishi wote katika swala zima la kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

"Napenda kuwatoa hofu watumishi wote kwa ujio wangu kwani nitawapa ushirikiano na kuwawezesha kutimiza majukumu yenu ikiwa ni pamoja na utoaji wa huduma bora ili kutimiza azma ya Serikali ya awamu ya tano ya kusikiliza na kuzitatua kero za wananchi pamoja na rasilimali za Tanzania ili kuwanufaisha wananchi wote hasa wanyonge na watoto wa maskini, nukuu nimekuja hapa kutimiza torati na si kuivunja" alisema Mhe. Muro. 

Alisisitiza kuwa ushirikiano huo utaanza kwa kuwapa fursa watumishi hao kwa kueleza changamoto zao na kupokea mawazo,maoni na mikakati itakayoleta maendeleo kwenye halmashauri hiyo na Wilaya ya Arumeru. Alibainisha kuwa anatarajia kufanya kikao kingine Jumatatu Agosti 6 2018.

 Awali aliyekuwa akikaimu nafasi hiyo ambaye ni mkuu wa wilaya ya Monduli Mhe. Idd Kimanta akimkabidhi ofisi hiyo alisema kuwa watumishi wa Meru ni wazuri na wachapakazi na amemkabidhi pamoja na ofisi wakiwa weupe na wenye afya tele pia wanyeyekevu.Mhe. Kimanta aliwawataka watumishi hao kumpa ushirikiano mkubwa mkuu huo mpya wa wilaya kama walivyompa yeye ili kuweza kuwaletea maendeleo wananchi wa meru na taifa kwa ujumla.
Mkuu wa wilaya ya Monduli Mhe. Idd Kimanta ambaye alikuwa akikaimu nafasi ya Ukuu wa Wilaya ya Arumeru akiongea kabla ya kukabidhi ofisi kwa DC mpya Mhe. Jerry Muro.
Sehemu ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Arumeru wakiwa kwenye kikao hico
Mkuu mpya wa wilaya ya Arumeru, Mhe. Jerry Muro akiongea kwenye kikao hicho

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...