Aliyekuwa Katibu Mkuu wa klabu ya Yanga, na mchezaji wa zamani wa timu ya Yanga na Taifa Stars  Charles Boniface Mkwasa afanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo.

Mkwasa yuko jijini New Delhi, India ambako amefanyiwa upasuaji huo mkubwa na imeelezwa bado yuko katika chumba cha usimamizi maalum, yaani ICU.

Mkwasa alisafiri takribani wiki moja iliyopita kwenda nchini India kwa ajili ya matibabu baada ya kugundulika na tatizo la moyo hapa nchini.

Mkwasa aliamua kujiuzulu nafasi yake ndani ya Yanga kwa ajili ya kujiuguza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...