Kampuni ya Multichoice inajivunia kuongeza chaneli mpya ya filamu inayojulikana kwa jina la Star Life mahususi kwa ajili ya wapenzi wa filamu na Tamthilia za kihindi.

Chaneli hii yenye maudhui ya kihindi inayorusha matangazo kwa Lugha ya kingereza imeanza rasmi kupatikana tarehe 27 Agosti 2018 chaneli namba DStv 167 iliyopo kuanzia kifurushi cha DStv Family.

Wateja wa DStv na watanzania wote kwa ujumla wataweza kufurahia filamu nzuri na za Kisasa za kihindi, Tamthilia na Series kali zenye kugusa hisia na tamaduni na maisha ya kihindi na vipindi vingine mbalimbali vya burudani kupitia chaneli hii vitakavyokuwa rushwa hewani kwa lugha ya kiingereza.

Kwa zaidi ya miaka 20 chaneli hii imekuwa ikipeperusha bendera kwa kuwa chaneli namba moja kutokana na ubora wa maudhui ya filamu na sinema zilizosheni ndani yake.

“Nyongeza ya chaneli hii ni matokeo ya kuhakikisha kuwa wateja wetu wanaendelea kufurahia huduma za DStv kwa burudani za kisasa kabisa ambazo hawatoweza kuzipata kwingine kokote. Chaneli hii itakuwa ikipatikana ndani ya DStv kupitia chaneli namba 167 kuanzia kifurushi cha Family 39,000.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...