Na WAMJW Dodoma
Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Bw. Marcel Katemba ameyataka wadau wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kutilia mkazo katika kutekeleza Sera za Maendeleo zilizopo katika Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto(Idara Kuu Maendeleo ya Jamii) ili kufanikisha juhudi za Serikali katika kuletea wananchi Maendeleo.
Ameyasema hayo wakati akifungua kikao cha ushirikiano baina ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yanayotekeleza Sera zinazosimamiwa na kuratibiwa na chini ya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii leo Jijini Dodoma.
Bw. Katemba amesisitiza kuwa Mashirika hayo yanapaswa kuwasilisha mipango yao kwa Msajili ili kuweza kuwa na Mpango mkakati mmoja wa kuwezesha kufanya kazi kwa ufanisi.
Ameongeza kuwa suala la Maendeleo ni mtambuka na linapaswa kutekelezwa kwa ushirikiano baina ya Serikali, Wadau na wananchi ili kufanya shughuli za Maendeleo kuwa endelevu.
Watendaji wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto kutoka Idara Kuu Maendeleo ya Jamii pamoja na wadau kutoka
Mashirika Yasiyo ya Kiserikali wakisikiliza mada zilizokuwa
zikiwasilishwa kuhusu ushirikiano kati ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali
na Serikali katika kikao cha ushirikiano baina ya Wizara ya Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na Mashirika Yasiyo ya
Kiserikali yanayotekeleza Sera zinazosimamiwa na kuratibiwa na chini ya
Idara Kuu Maendeleo ya Jamii. Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano
WAMJW
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Bw. Marcel Katemba ameyataka wadau wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kutilia mkazo katika kutekeleza Sera za Maendeleo zilizopo katika Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto(Idara Kuu Maendeleo ya Jamii) ili kufanikisha juhudi za Serikali katika kuletea wananchi Maendeleo.
Ameyasema hayo wakati akifungua kikao cha ushirikiano baina ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yanayotekeleza Sera zinazosimamiwa na kuratibiwa na chini ya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii leo Jijini Dodoma.
Bw. Katemba amesisitiza kuwa Mashirika hayo yanapaswa kuwasilisha mipango yao kwa Msajili ili kuweza kuwa na Mpango mkakati mmoja wa kuwezesha kufanya kazi kwa ufanisi.
Ameongeza kuwa suala la Maendeleo ni mtambuka na linapaswa kutekelezwa kwa ushirikiano baina ya Serikali, Wadau na wananchi ili kufanya shughuli za Maendeleo kuwa endelevu.
Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Bw. Marcel Katemba akizungumza
na wadau wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Jijini Dodoma katika kikao
cha ushirikiano baina ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yanayotekeleza Sera
zinazosimamiwa na kuratibiwa na chini ya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...