Na Andrew Chale, Dar

Tamasha kubwa na la aina yake la muziki wa Kiafrika maalum kumuenzi gwiji wa muziki Hayati Dk. Remmy Ongala lililopewa jina la ONGALA MUSIC FESTIVAL, linatarajiwa kulindima kwa mara ya kwanza kuanzia hapo kesho katika fukwe mwanana za Malaika Beach Club, Kigamboni, Agosti 23-25.

Akizungumza Mratibu wa tamasha hilo Bi. Aziza Ongola anaesimamia mfuko wa Ongala (Ongala Foundation), amesema tayari maandalizi yote yameenda vizuri na watu wakae mkao wa kulishuhudia tamsha hilo ambalo ni la urithi wa muziki kutoka kwa gwigi Dk. Remmy.

Aziza amesema kuwa, Wasanii mbalimbali kutoka Nchi tofauti za Afrika na bendi zao watatoa burudani kwa muda wa siku tatu yaani kuanzia Agosti 23-25,2018 katika fukwe hizo za Malaika, Kigamboni.

“Tutamuenzi Baba kupitia nyimbo zake nyingi ambazo zimekuwa na umaarufu ndani na nje ya Afrika. Hivyo tamasha ili ni kuamsha hali ya Muziki aliouacha na pia kuendelea kumkumbuka kupitia mashairi yake” alieleza Aziza.Aziza ameongeza kuwa, tamasha hilo pia litasaidia kuimarisha kumbukumbu na kazi za gwiji huyo aliyefariki Desemba 2010, Nchini.

Kwenye tamasha hilo vikundi 22 kutoka nchi mbalimbali za Afrika vitatumbuiza kwa siku hizo tatu.Miongoni mwa wasanii hao ni msafiri Zawose, Ally Swahi, Siti and the Bend, Hokororo, King kiki na Sikinde. Pia atakuwepo Ashimba, Carola Ongala Music Festival kulindima kesho Agosti 23-25,Kigamboni

Tamasha kubwa na la aina yake la muziki wa Kiafrika ambalo ni maalum kumuenzi gwiji wa muziki Hayati Dk. Remmy Ongola lililopewa jina la ONGALA MUSIC FESTIVAL, linatarajia kulindima kwa mara ya kwanza kuanzia hapo kesho katika fukwe mwanana za Malaika Beach Club, Kigamboni.

Akizungumza Mratibu wa tamasha hilo Bi. Aziza Ongola anaesimamia mfuko wa Ongala (Ongala Foundation), amesema tayari maandalizi yote yameenda vizuri na watu wakae mkao wa kulishuhudia tamsha hilo ambalo ni la urithi wa muziki kutoka kwa gwigi Dk. Remmy.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...