JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU
Simu: 255-22-2114512, 2116898
Baruapepe: press@ikulu.go.tz
Nukushi: 255-22-2113425 |
OFISI YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, atafanya ziara ya kikazi katika mikoa ya Mwanza, Mara na Simiyu kati ya tarehe 03 Septemba, 2018 na tarehe 10 Septemba, 2018.
Katika ziara hiyo Mhe. Rais Magufuli ataweka mawe ya msingi na kufungua miradi mbalimbali ya maendeleo, pamoja na kuzungumza na wananchi katika mikutano ya hadhara.
Taarifa zaidi kuhusu ziara ya Mhe. Rais Magufuli katika mikoa husika zitatolewa na viongozi wa mikoa hiyo.
Aidha, baada ya kumaliza ziara katika mikoa hiyo Mhe. Rais Magufuli anatarajia kufanya ziara katika mikoa ya Katavi, Rukwa, Songwe na Mbeya katika tarehe zitakazopangwa.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Chato, Geita
30 Agosti, 2018
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...