Kampuni
ya michezo ya kubashiri SportPesa na Klabu ya mpira wa miguu ya
Uingereza ya Everton zimezawadiwa zawadi kutokana na ushirikiano wao
kwenye tuzo za Sports Industry Awards kwenye vipengele vya Best African
Sponsorship na Pan-African Campaign of the year.
Kwenye udhamini huo ambao ulianza kwa klabu ya Everton kusafiri kwenda Dar es Salaam Julai 2017 kucheza na Mabingwa wa SportPesa Super Cup ambao walikuwa klabu ya Gor Mahia kutoka Kenya, umetambuliwa na kusherekewa kwa kuwaleta Everton wanaoshiriki ligi kuu ya Uingereza kwenye Ukanda wa Afrika Mashariki kwa mara ya kwanza.
Kutokana na mafanikio ya safari hiyo ambayo ilijulikana kama 'Everton in Tanzania' , ambayo pia ilileta hamasa kwenye michezo na kuipa ushindi wa tuzo hizo ambazo zilitangazwa Sandton Convention Centre jijini Johannesburg Ijumaa ya tarehe 17 Agosti 2018.
Mkuu wa Ushirikiano na Utawala wa klabu ya Everton Mark Rollings alisema "Tunayo furaha kuwa ushirikiano wetu na SportPesa umetambulika kwenye ngazi muhimu ya Sports Industry Awards. Tuzo za Sports Industry Awards ndio tuzo zenye heshima kubwa Afrika Kusini kwa upande wa michezo na kwa hivyo kushinda tuzo zote mbili za Best African Sponsorship na Pan-African Campaign of the Year ni udhibitisho wa kuendeleza ushirikiano wetu na SportPesa pamoja na wadau wake.
Kwenye udhamini huo ambao ulianza kwa klabu ya Everton kusafiri kwenda Dar es Salaam Julai 2017 kucheza na Mabingwa wa SportPesa Super Cup ambao walikuwa klabu ya Gor Mahia kutoka Kenya, umetambuliwa na kusherekewa kwa kuwaleta Everton wanaoshiriki ligi kuu ya Uingereza kwenye Ukanda wa Afrika Mashariki kwa mara ya kwanza.
Kutokana na mafanikio ya safari hiyo ambayo ilijulikana kama 'Everton in Tanzania' , ambayo pia ilileta hamasa kwenye michezo na kuipa ushindi wa tuzo hizo ambazo zilitangazwa Sandton Convention Centre jijini Johannesburg Ijumaa ya tarehe 17 Agosti 2018.
Mkuu wa Ushirikiano na Utawala wa klabu ya Everton Mark Rollings alisema "Tunayo furaha kuwa ushirikiano wetu na SportPesa umetambulika kwenye ngazi muhimu ya Sports Industry Awards. Tuzo za Sports Industry Awards ndio tuzo zenye heshima kubwa Afrika Kusini kwa upande wa michezo na kwa hivyo kushinda tuzo zote mbili za Best African Sponsorship na Pan-African Campaign of the Year ni udhibitisho wa kuendeleza ushirikiano wetu na SportPesa pamoja na wadau wake.
Meneja
masoko SportPesa South Afrika Gail Rodgers, Mkuu wa kitengo cha masoko
SportPesa Kelvin Twissa, Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni
na Michezo Susan Mlawi, Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti SportPesa
Tanzania Tarimba Abbas na Mkuu wa kitengo ca Ushirikiano Everton Mark
Rollings mara baada ya kukabidhiwa tuzo za Sport Industry Awards.
Wawakilishi
kutoka SportPesa Tanzania, Kenya, South Africa,Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Tanzania, Timu ya Everton wakipokea tuzo
mara baada ya kutangazwa kuwa washindi.
Katibu
wa wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Susan Mlawi akiwa na
Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti SportPesa Tanzania Tarimba Abbas
wakiwa na tuzo mbili za Sport Industry Awards ambazo kampuni ya
SportPesa imeshinda kwenye vipengele vyote viwili.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...