Mkurugenzi wa Magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akielezea maendeleo ya ukarabati wa jengo la watoto kwa Naibu Balozi wa Marekani nchini Mhe. Dkt. Inmi Patterson (wa pili kulia) alipotembelea Taasisi hiyo leo kwaajili ya kuona kambi maalum ya matibabu ya moyo inayofanywa na madaktari wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka Marekani (Madaktari Afrika).
Naibu Balozi wa Marekani nchini Mhe. Dkt. Inmi Patterson akitoka kuangalia ukarabati wa jengo la watoto la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea Taasisi hiyo leo kwaajili ya kuona kambi maalum ya matibabu ya moyo inayofanywa na madaktari wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka nchini Marekani (Madaktari Afrika).
Naibu Balozi wa Marekani nchini Mhe. Dkt. Inmi Patterson akiongea jambo na madaktari kutoka Marekani (Madaktari Afrika) walioko katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kambi maalum ya matibabu kwa wagonjwa wenye matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo. Jumla ya wagonjwa nane wameshafanyiwa matibabu katika kambi hiyo na hali zao zinaendelea vizuri.
Naibu Balozi wa Marekani nchini Mhe. Dkt. Inmi Patterson akimsalimia mtoto Catherine Mapunda ambaye amefanyiwa upasuaji wa moyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Mhe. Patterson alitembelea Taasisi hiyo leo kwaajili ya kuona kambi maalum ya matibabu ya moyo inayofanywa na madaktari wa JKCI kwa kushirikiana na wataalam kutoka nchini Marekani (Madaktari Afrika).KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...