Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mipango ya Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi isiyo ya kiserikali ya YES, Kenneth Simbaya (kulia) mipira itakayotumika kufunza vijana kuhusu SDGs na wajibu katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi isiyo ya kiserikali ya YES, Kenneth Simbaya (katikati) akimkabidhi Necta Mussa (kulia) kijana ambaye aliwakilisha wenzake mipira itakayotumika kufunza vijana hao kuhusu SDGs na wajibu wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Dar es Salaam. Anayeshuhudia tukio hilo ni Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mipango ya Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (kushoto).
Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi isiyo ya kiserikali ya YES, Kenneth Simbaya (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) mara baada ya kupokea mipira hiyo ya kuhamasisha vijana kuhusu SDGs na wajibu kupitia michezo wakati wa hafla fupi ya makabidhiano hayo iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwakilishi wa vijana kutoka YES Necta Mussa na kushoto ni Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mipango ya Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...