Na Frankius Cleophace Serengeti
WAZAZI na walezi Wilayani Serengeti mkoani mara wametakiwa kuachana na suala la ubaguzi katika mgawanyo wa majukumu ya kazi majumbani ili kuleta usawa wa kijinsia huku mtoto wa kike akilimbikiziwa kazi nyingi kuliko mtoto wa kiume majumbani. 

Hayo yamebainishwa na wanafunzi katika tamasha la kutoa elimu juu ya masuala ya kupinga Mila na desturi zilizopitwa nawakati ukiwemo Ukeketaji, Ndoa za Utotoni pamoja na mimba za utoto tamasha lililoandaliwa na Shirika la RIGTH TO PLAY nakushirikisha shule za Msingi Nyamisingisi,Nyiberekera kata ya Isenye Wilayani Serengeti Mkoani Mara.

Elizabert Kirinda ni mwanafunzi wa shule ya msingi Nyamisingisi amesema kuwa majumbani watoto wa kike wamekuwa wakipewa kazi nyingi za kufanya kuliko watoto wa kiume jambo amabalo linachangia kukosa muda mwingi wa kijisomea wao kama mabinti hivyo wameomba wazazi na walezi kutoa mgawanyo sawa wa kazi ili kuondoa ubaguzi wa jinsia.

“Sisi wasichana majumbani tunapewa kazi nyingi kupika, kuchota maji kulea watoto na wavula hawafanyi kazi zozote na wakati mwingine tunachunga mifugo hatuna muda wa kusoma tukiwa nyumbani tunaomba wazazi waweze kugawanya sawa majukumu ya kazi majumbani” alisema Elizabert.
 Picha 1 ni Wanafunzi wa shule ya msingi Nyiberekera pamoja na shule ya msingi Nyamisingisi wakiwa katika maandamano kwa lengo la kufikisha ujumbe kupitia mabango mabalimbali waliyobeba kabla ya kuanza kwa Tamasha hilo.
 Wanafunzi wa shule ya msingi Nyamisingisi wakiimba wimbo ulibeaba ujumbe wa kupiga vita ukatili kwa watoto.
 Leah Kimaro ambaye ni mwezeshaji kutika shirika la RIGHT TO PLAY akitoa elimu juu ya madhara ya ukatili wa kijinsia katika Tamasha hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...