Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto) akimkabidhi taarifa za Baraza jipya la Taifa la Usalama Barabarani, mjumbe aliyeteua, Profesa Zakaria Mganilwa. Katikati ni Katibu Mtendaji wa Baraza hilo ambaye pia ni Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Fortunatus Musilimu. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akiyasoma majina ya wajumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani katika ukumbi wa mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dodoma leo. Lugola aliwataka wajumbe hao wahakikishe wanadhibiti ajali za barabarani nchini. Kushoto meza kuu ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali, Jacob Kingu.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akizungumza na wajumbe wa Baraza jipya la Taifa la Usalama Barabarani mara baada ya Baraza hilo kuzinduliwa katika ukumbi wa mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dodoma leo. Lugola aliwataka wajumbe hao wahakikishe wanadhibiti ajali za barabarani nchini. Kushoto meza kuu ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali, Jacob Kingu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kulia meza kuu), akimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Jacob Kingu alipokua akifafanua masuala ya usalama barabarani, kabla ya Waziri Lugola kulizindua Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, katika ukumbi wa wizara, jijini Dodoma leo
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...