Na.
Vero Ignatus Ngorongoro
OXFAM
kwa kushirikiana na Shirika la PALISEP wameendesha mafunzo
ya teknolojia ya kidigitali kwa wananchi wilaya ya Ngorongoro
mkoani Arusha ili kuleta maendeleo katika jamii husika.
Maratibu
wa Teknolojia kwa maendeleo shirika la Oxfam Bill Marwa amesema
wametoa mafunzo kwa wananchi zaidi ya (90)yakiwa na lengo la wao
kutambua namna ya kuitumia mitandao hiyo pamoja nyenzo
mbalimbali za kidigital kwa kutuma ujumbe mfupi, kutoa taarifa kwa
viongozi wao wa kijiji,kujibuwa changamoto wanazokutana nazo kwaajili
ya kujiletea maendeleo.
"Kadri miaka inavyoenda
kumekuwa na ongezeko la mitandao ya kijamii ulimwenguni hivyo Oxfam kama
shirika limeona upo umuhimu wa maendeleo, kupata taarifa, kutoa
matokeo"alisema Bill Marwa.Washiriki
wa mafunzo hayo walifundishwa sheria za mtandao 2015 pamoja na makosa
ya mtandaoni, jinsi ya kutumia vifaa hivyo katika namna ambayo
havivunji sheria ya nchi.
Sambamba
na hayo walifundishwa maswala Mbalimbali jinsi ya ukingi haswa kwa
wanawake kulinda haki za mwanamke na kupinga ukatili wa kijinsia dhidi
yao.Mafunzo
hayo yaliyokuwa ya siku nne yaliyoshirikisha kata zaidi ya 10
katika wilaya ya Ngorongoro,ikiwa ni mradi wa miaka miwili
unaotekelezwa katika mikoa (4) Arusha, Geita,Kigoma,na Mtwara katika
wilaya za Mtwara vijijini, Mbogwe Geita, Kibondo,na
Ngorongoro.
Mradi huo
unalengo la kuwawezesha wananchi kutumia nyenzo za digitali ili
kujiletea maendeleo katika jamii husika,amabapo ulianzishwa rasmi
mwaka 2016 desemba na unatarajiwa kumalizika novemba 2018 ,mradi huo
upo chini ya ufadhili kutoka nchini Ubelijiji.
Meneja wa Program Shirika la Oxfam
Kefar Mbogela akitoa Elimu namna ya kutumia mitandao na nyenzo
mbalimbali za kidigitali bila kuleta madhara kwa jamii wala kuvunja
sheria ya mitandao hiyo
Rachel yeye anasema mwanzoni
alikuwa akitumia simu ya hali ya chini ambayo alikuwa hapati mambo
mengi ya faida ,ila kwa sasa mara baada ya kupewa simu na Oxfam
imemsaidia sana kuweza kuwasiliana na na jamii ,amesema kwasasa
anaweza kupaza sauti kwa kutumia simu yake,kutatua changamoto
mbalimbali na viongozi wanapoona ujumbe wake wanatatua tatizo na
majibu yanapatikana kwa wakati.
Darasa la mafunzo ya kutumia nyenzo
za mitandao ya kijamii na namna ya kutumia nyenzo za kidigitali
yakiendelea.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...