Kampuni ya Acacia Mining PLC kupitia migodi yake ya Buzwagi na Bulyanhulu imeshiriki maonyesho ya Teknolojia Bora ya Uzalishaji Dhahabu kwa Maendeleo ya Kijamii na Uchumi wa Viwanda yanayofanyika katika viwanja vya Kalangalala Mkoani Geita.
Akizungumzia Ushiriki wa Migodi ya Acacia ya Bulyanhulu na Buzwagi Mhandisi wa Uchenjuaji wa Bulyanhulu Emmanuel Muchunguzi amesema katika Maonyesho hayo wamejipanga kuielimisha jamii kuhusu uchimbaji wa madini chini ya ardhi, hatua za Uchenjuaji wa Dhahabu, masuala ya Mazingira, Afya, na usalama mahala pa kazi.
Muchunguzi amewakaribisha wadau mbalimbali waweze kutembelea banda la Maonyesho la Acacia ili wajifunze masuala mbalimbali hasa ya kuhusu uchimbaji na Uchenjuaji salama kwani usalama ndiyo nguzo muhimu ya Uzalishaji wa Dhahabu. Maonyesho hayo yameandaliwa na Mkoa wa Geita.
Wakazi wa Geita wakiwa katika banda la Kampuni ya Uchimbaji madini ya Acacia kwenye maonyesho
ya Teknolojia Bora ya Uzalishaji Dhahabu kwa Maendeleo ya Kijamii na
Uchumi wa Viwanda yanayofanyika katika viwanja vya Kalangalala Mkoani
Geita.Picha zote na Mary Lupamba - Acacia
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...