Na Mwandishi Wetu
Wajasiriamali nchini wametakiwa kujiamini kuwa wanaweza kuletea maendeleo kwa kugundua na kutumia ipasavyo fursa za uwekezaji zilizopo nchini.
Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dk Reginald Mengi kwenye mazungumzo na wajasiriamali wa Asasi ya Entrepreneur Organization – EO Tawi la Tanzania, waliomwalika awasimulie uzoefu wake katika ujasiriamali na kuhusu Kitabu alichokitunga.
Amesema Watanzania hawana budi wajiamini kuwa kwa jitihada zao wanaweza kujikwamua kiuchumi kwa kuwekeza kwenye fursa anuwai zilizopo nchini, wakati huu ambapo Rais John Magufuli anahamasisha uwekezaji, hususan wa viwanda, baada ya kuboresha mazingira ya uwekezaji.
Alisema hilo linawezekana kwa kujifunza kusema kwamba nitaweza na lazima na kisha kutekeleza uthubutu huo kivitendo.
Alisema kwamba yeye akiwa anatoka katika familia maskini aliweza kufanikisha kuwa mfanyabiashara mkubwa kutokana na dhamira yake ya kusema nitaweza na kutekeleza msemo huo kwa vitendo.
Aidha alisema aliandika kitabu hicho kama alivyoshauriwa na mtoto wake Rodney ili kuwashawishi watanzania wengi zaidi kuwa na uthubutu na ushauri katika kujikita kwenye ujasiriamali na kutumia fursa.
Aidha aliwataka watanzania kujifunza na kuwa wabunifu na watunga sera kuona kama elimu yetu ya sasa inakidhi mahitaji halisi au inatakiwa kuboreshwa ili kusaidia katika harakati za kuipeleka nchi yetu kwenye uchumi wa kati.
Alisema hayo wakati akijibu maswali katika mdahalo huo kuhusu elimu na kama elimu yetu inafaa kwa sasa.
Alisema kitabu alichotunga kinaelezea uzoefu wake katika ujasiriamali kutokana na ukweli kuwa hata wakati wa kuanzisha IPP ni kuwezesha ubunifu na teknolojia miongoni mwa watanzania.
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dk. Reginald Mengi akizungumza na
wajasiriamali wa Asasi ya Entrepreneur Organization – EO Tawi la
Tanzania, waliomwalika awasimulie uzoefu wake katika ujasiriamali na
kuhusu Kitabu alichokitunga ‘I Must, I Can, I Will-The Spirit of
Success’ alipokutana nao Hoteli ya Coral Beach, Masaki jijini Dar es
Salaam. Kushoto ni Mwenyekiti wa Mafunzo wa Asasi ya EO tawi la
Tanzania, Bi. Miranda Naiman.
Mmoja wa wajasiriamali hao ambao ni wamiliki wa makampuni mbalimbali
nchini akiuliza swali kwa Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dk. Reginald Mengi
(hayupo pichani) wakati wa mazungumzo na wajasiriamali wa Asasi ya
Entrepreneur Organization – EO Tawi la Tanzania, waliomwalika awasimulie
uzoefu wake katika ujasiriamali na kuhusu Kitabu alichokitunga ‘I Must,
I Can, I Will-The Spirit of Success’ alipokutana nao Hoteli ya Coral
Beach, Masaki jijini Dar es Salaam.
Wajasiriamali wa Asasi ya Entrepreneur Organization – EO Tawi la
Tanzania, wakimsikiliza Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dk. Reginald Mengi
(hayupo pichani) alipokuwa akiwasimulia uzoefu wake katika ujasiriamali
na kuhusu Kitabu alichokitunga ‘I Must, I Can, I Will-The Spirit of
Success’ alipokutana nao Hoteli ya Coral Beach, Masaki jijini Dar es
Salaam.
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dk. Reginald Mengi akitia saini nakala za
kitabu chake ‘I Must, I Can, I Will-The Spirit of Success’
zilizonunuliwa na wajasiriamali hao ambao ni wamiliki wa makampuni
mbalimbali nchini mara baada ya mazungumzo yaliyofanyika katika hoteli
ya Coral Beach-Masaki, jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dk. Reginald Mengi katika picha ya pamoja na
wajasiriamali wa Asasi ya Entrepreneur Organization – EO Tawi la
Tanzania huku wakiwa wameshika nakala za kitabu chake ‘I Must, I Can, I
Will-The Spirit of Success’ mara baada ya mazungumzo yaliyofanyika
katika hoteli ya Coral Beach-Masaki, jijini Dar es Salaam.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...