Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akisalimiana na Balozi wa Jamhuri ya Kenya Nchini Tanzania Mhe.Dan Kazungu alipofika kujitambulisha leo Ikulu Mjini Zanzibar akifuatana na ujumbe wake.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amesema kuwa Kenya na Zanzibar zinauhusiano wa kihistoria hivyo ushirikiano katika sekta ya biashara kati ya pande mbili hizo utakuza uchumi na kuuendeleza udugu wa damu uliopo.

Dk. Shein aliyasema hayo leo, Ikulu mjini Zanzibar wakati alipofanya mazungumzo na Balozi mpya wa Kenya katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dan Kazungu aliyefika Ikulu kwa ajili ya kujitambulisha. Katika mazungumzo hayo, Dk. Shein alimueleza Balozi Kazungu kuwa Zanzibar na Kenya zina uhusiano na ushirikiano wa kihistoria hasa katika sekta ya biashara ambapo Zanzibar ilikuwa ndio kitovu kikuu cha biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki tokea karne ya 19.

Dk. Shein alieleza kuwa kuna kila sababu ya kuimarisha uhusiano na ushirikiano kati ya Zanzibar na Kenya katika kuimarisha sekta mbali mbali za maendeleo ambapo kwa upande wa sekta ya biashara ndio sekta pekee yenye historia kati ya pande mbili hizo. Alisema kuwa wananchi wa Kenya na Zanzibar wana udugu wa damu na kutokana na matukio kadhaa ya kihistoria yakiwemo Watawala waliozitawala nchi hizo yamejenga ukaribu mkubwa na kumpelekea Dk. Shein kusisitiza haja ya kuimarisha uhusiano na ushirikiano uliopo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Kenya Nchini Tanzania Mhe.Dan Kazungu alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo kujitambilisha akiwa na ujumbe wake (hawapo pichani).

Katika maelezo yake, Rais Dk. Shein aliunga mkono wazo la Balozi huyo wa Kenya la kuwekwa utaratibu maalum wa kuzidisha ushirikiano huo katika sekta za maendeleo ikiwemo sekta ya biashara kati ya Kenya na Zanzibar kwa lengo la kukuza uchumi na kuinua ustawi wa maisha ya wananchi wa pande mbili hizo.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...