Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine Kasike (mwenye miwani)
akisalimiana na baadhi ya maafisa wa ofisi ya Mkuu wa Magereza mkoa wa
Tanga, Gereza Kuu Maweni na gereza la Mahabusu Tanga mara alipowasili katika
viwanja vya Gereza Kuu Maweni jijini Tanga akiwa katika ziara ya kikazi ya siku
moja mkoani humo leo Septemba 7, 2018.
Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine Kasike (mwenye
“microphone” ) akizungumza na maafisa na askari wa vituo vya ofisi ya Mkuu wa
Magereza Mkoa wa Tanga, Gereza Kuu Maweni na Gereza la Mahabusu Tanga
(hawapo pichani) kwa pamoja katika bwalo la Gereza Kuu Maweni Tanga
alipofanya ziara ya siku moja ya kikazi mkoani humo. Wa kwanza kulia ni Kaimu
Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP)
Emmauel Lwinga, wa tatu kulia ni Mkuu wa Gereza Kuu Maweni Kamishna
Msaidizi wa Magereza (ACP) Felichism Masawe na wa kwanza kushoto ni Afisa
Mnadhimu wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga Marakibu Mwandamizi wa
Magereza (SSP) Hamis Mbwana.
Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine Kasike akifuatilia kwa
makina taarifa ya mkoa wa Tanga kutoka kwa Kaimu Mkuu wa Magereza wa
Mkoa huo Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Emmanuel Lwinga alipofanya
ziara ya kikazi ya siku moja mkoani humo leo Septemba 7,2018.
Baadhi ya maafisa na askari wa vituo vya ofisi ya Mkuu wa Magereza
mkoa wa Tanga, waliokusanyika kwa pamoja katika bwalo la gereza Kuu Maweni
wakifuatilia kwa makini hotuba ya Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine
Kasike (hayupo pichani) alipofanya ziara ya kikazi mkoani humo leo Septemba 7,
2018. Katika hotuba yake CGP ametilia mkazo suala la kubadili mtazamo wa
kiutendaji, kuacha kufanya kazi kwa mazoea ili kufanikisha majukumu yetu kama
serikali na jamii nzima inavyotarajia kutoka kwetu.
Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine Kasike akiwa katika
picha ya pamoja na baadhi askari wa magereza wa kike mkoani Tanga alipofanya
ziara ya siku moja mkoani humo leo Septemba 7, 2018.
Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine Kasike akiwa katika
picha ya pamoja na baadhi ya askari wa Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia
Magerezani (KMKGM) walioko mkoani Tanga alipofanya ziara ya kikazi ya siku
moja mkoani humo leo Septemba 7, 2018.
Picha zote na Jeshi la Magereza.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...