Kiongozi Mkuu wa Kituo cha Afya cha PCMC Richard Ulanga akizungumza na waandishi habari mara baada ya Kituo hicho kutoa msaada katika Kituo cha Afya Vijibweni,Kigamboni Jijini Dar es Salaam
 Kiongozi Mkuu wa Kituo cha Afya cha PCMC Richard Ulanga akikabidhi msaada katika mgonjwa aliyelazwa katika Kituo cha Afya Vijibweni.
Picha ya watumishi wakiwa wameshika vitu vya msaada kwa ajili ya wagonjwa waliopo katika Kituo cha Afya Vijibweni.


Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
KITUO cha Afya cha PCMC kimetoa msaada wa vifaa mbalimbali katika kituo cha Afya Vijibweni, Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari Viongozi Mkuu wa Kituo hicho Richard Ulanga amesema msaada huo ulilengwa kwa wagonjwa katika kutuo cha Vijibweni ikiwa ni maadhimisho ya miaka mitano ya kituo cha Afya cha PCMC.
Amesema kama watoaji wa huduma za afya wameona na umuhimu wa kutoa msaada katika kituo cha afya cha Serikali.
Ulanga amesema hawataishia hapo bali wataendelea kutoa msaada kila wanapoadhimisha miaka mingine
Aidha amesema katika kusherekea huko kila mtumishi amejitoa kwa nafasi yake kwa kutambua anawajibu ya kusaidia jamii inayomzunguka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...