Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson M. Masilingi, akizungumza wakati akisoma hotuba kwa niaba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim M. Majaliwa, aliyekuwa amealikwa kufungua Kongamano la Watanzania wanaoishi Marekani, lililoandaliwa na DICOTA (Diaspora Council of Tanzanians in America) tarehe 31 Agosti, 2018 hadi tarehe 2 Septemba, 2018 Seattle, Marekani.
Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba John Kabudi, akiwasilisha hotuba yake kuhusu tulipotoka baada ya Uhuru, tulipo sasa, tunapoelekea, mafanikio na mipango ya Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Washiriki wa Kongamano la Diaspora, Marekani wakishangilia hotuba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyoshehini mafanikio na mipango kabambe ya Serikali ya Awamu ya Tano.
Washiriki katika Kongamano la Jumuiya ya Watanzania waishio Marekani lililoandaliwa na DICOTA (Diaspora Council for Tanzanians in America), wakifuatilia Hotuba hiyo katika Hoteli ya Seattle Marriott Belleview, Seattle, Washington, Marekani tarehe 31 Agosti 2018 hadi tarehe 2 Septemba 2018.
Picha ya pamoja ya Ujumbe wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika Kongamano la Diaspora, Seattle, Washington, Marekani na viongozi wa DICOTA wenyeji wa Kongamano hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...