Na Said Mwishehe,Globu ya Jamii

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amesema kukamilika kwa Flyover ya Mfugale iliyopo Tazara kutasaidia kunusuru ndoa za watu wa mkoa huo.

Makonda amesema hayo leo mbele ya Rais Dk.John Magufuli wakati wa uzinduzi wa Flyover  ya Mfugale iliyopo makutano ya Tazara jijini Dar es Salaam ambapo amesema kwamba kukamilika kwa Flyover hiyo ni wazi sasa wananchi wanaondokana na changamoto ya foleni kubwa.

"Kuna ndoa za watu zimeingia kwenye kutoaminiana kwa sababu tu ya msongamano wa magari makutano ya Tazara.Wapo waliokuwa wanachelewa kurudi nyumbani na wakiulizwa na wenza wao wanasingizia foleni.

" Kuna baadhi yao walikuwa wanatumia foleni ya Tazara kama kificho kwani wanakwenda gesti na wakiulizwa wanasema walikuwa kwenye foleni,"amesema Makonda na kuongeza kwamba

"Sasa kuanza kutumika kwa flyover hii kutaimarisha ndoa kwani hakutakuwa na visingizio tena,"amesema Makonda huku akitumia nafasi hiyo kufikisha salamu za wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa Rais.

Pia amesema flyover hiyo itarahisisha shughuli za kiuchumi kwa mkoa wa Dar es Salaam ambapo ameeleza kufurahishwa kwake na namna ambavyo Rais Magufuli amedhamiria kuboresha maisha ya wananchi na hiyo imesababisha Watanzania kutembea kifua mbele.

Makonda ametumia nafasi hiyo kuelezea namna ambavyo Rais Magufuli ameendelea kuboresha miundombinu ya Jiji la Dar es Salaam kwani kuna barabara nyingi ujenzi unaendelea.Amesema kuna miradi mingi ya maendeleo ambayo inaendelea kujengwa ambapo amesema kuna kilometa chache ambazo zimesalia.

Makonda amesema kutokana na kazi kubwa ambayo inaendelea kufanyika wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam ombi lao ni moja tu ambalo ni Rais kufanya ziara katika mkoa huo.

"Nafikisha ujumbe wa wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam ni kwamba wanatamani kukuona ukipita kwenye mitaa yao na hivyo kiu na hamu yao ni kukuomba ufanye ziara ili uwatembelee nao wakuone",amesema Makonda.

Kwa upande wake Mkurugenzi  Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Japan(JICA)nchini Tanzania Toshio Nagase amesema kukamilika kwa Flyover ya Mfugale kutasaidia kuboresha maisha ya watu wa Dar es Salaam na nchi jirani.

Pia amesema awali ukitaka kwenda Uwanja wa Ndege walikuwa wanaondoka mapema katikati ya Jiji kwa sababu ya makutano ya Tazara lakini sasa wanaweza kuchelewa kuondoka kwa sababu ya daraja la juu la Mfugale

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...