Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia wananchi wa Musoma waliokusanyika katika viwanja vya Mukendo vilivyopo Musoma mjini kwa ajili ya kumsikiliza mara baada ya kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Mara.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Maji Profesa Makame Mbarawa, mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Ufaransa AFD Stephanie Mouen wakanza kulia mwenye wakivuta utepe kuashiria ufunguzi wa mradi wa maji safi na usafi wa mazingira katika manispaa ya Musoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Stephanie Mouen mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Ufaransa AFD Agence Francaise De Development waliosaidia katika mradi huo wa maji Musoma mkoani Mara.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akivuta utepe pamoja na Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isaack Kamwelwe wakivuta utepe kuashiria ufunguzi wa barabara ya kutoka Mpakani mwa Simiyu/Mara na Musoma km 85.5.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia dawati ambalo alikuwa akilitumia kujisomea Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika Shule ya Msingi Mwisenge Musoma. Hayati Mwalimu Nyerere alisoma shule hapo elimu ya Msingi tarehe 20/4/ 1934 hadi 1/10/1936.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...