NA FREDY MGUNDA,IRINGA
MKUU wa mkoa wa Iringa amepiga marufuku wafanyabiashara wadogo wadogo kunyanyaswa katika mahali ambazo wanafanyia biashara kwa kuwa wanatoa kodi ambayo inachochea kuleta maendeleo ya watanzania hususani mkoani iringa tukielekea kuijenga Iringa mpya.

Akizungumza kwenye mkutano na wafanyabiasha wadogodogo wa manispaa ya Iringa mkuu wa mkoa Ally Hapi alisema kuwa wafanyabiasha wadogo wadogo maarufu kama machinga wanatakiwa kufanya biashara zao kwa kufuta taratibu na sheria za nchi huku viongozi wakiancha kuwanyanyasa kwa kuwa nao ni wafanyabiashara.

“Toka nikiwa mkuu wa wilaya najua umuhimu wafanyabiasha wadogo wadogo kwa kuchangia katika kukuza uchumi wa eneo husika hivyo natangaza rasmi ni marufuku kuwanyanyasa wafanyabiasha wadogo wadogo wa mkoa wa Iringa” alisema Hapi

Hapi aliwataka polisi wanasimamia eneo lastand kuu kuacha mara moja kunyanyasa wafanyabiasha wadogo wadogo wanaofanyia biashara katika eneo hilo.
Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akiongea na wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama machinga wa manispaa ya Iringa kwa lengo la kusikiliza kero na changamoto ambazo wanakabiliana katika kuleta maendeleo ya mkoa wa Iringa na kuhakikisha wanaijenga Iringa mpya ambayo inatakiwa na wanairinga 
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akiongea wakati wa kikao cha wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama machinga na mkuu wa mkoa wa Iringa
Baadhi ya wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama machinga walijitokeza kumsikiliza mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi na kama ambavyo unawaona walivyokuwa makini kumsikiliza hapo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...