Sehemu ya waokoaji wakiwa katika pemezoni mwa kivuko cha Mv. Nyerere kilichopinduka na kupelekea idadi kubwa ya watu kupoteza maisha na wengine kujerukiwa, katika eneo la Ukara, Kisiwa cha Ukerewe jijini Mwanza, wakiangalia maeneo mbalimbali kutafuta miili au watu waliohai waliozama kwenye maji. ajali ya Kivuko cha MV. Nyerere kinachofanya safari zake kati ya Bugorora na Ukara katika wilayani ya Ukerewe mkoani Mwanza kilipinduka juzi Alhamisi (Septemba 20, 2018) kikikadiriwa kubeba idadi kubwa ya abiria kuzidi uwezo wake. Kwa Mujibu wa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Isack Kamwelwe, Mpaka wakati huu miili ya waliopolewa majini imefikia 209, huku kati yao miili  172 imetambuliwa huku 112 ikiwa imechukulia na ndugu zao.
 Picha zote na Steve Magombea.k.a Kasampaida.
 Vivuko vya Mv. Clarias na Mv. Nyehunge vikiwa tayari kwa msaada wowote wa hata.
 Baadhi ya vijana wa Skaut wakiwa wamebeba moja ya miili iliyoopolewa kwenye maji baada ya Kivuko cha MV. Nyerere kinachofanya safari zake kati ya Bugorora na Ukara katika wilayani ya Ukerewe mkoani Mwanza kilipinduka.
Zoezi la Ukoaji likiendelea.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...