Wafanyabiashara wa Tanzania wamehamasishwa kushiriki maonyesho ya Kimataifa ya Biashara katika Jimbo la Gujarat nchini India ili kupata fursa ya kufanya biashara na uwekezaji.
Hayo yamezungumzwa katika mkutano mkubwa wa wafanyabiashara kutoka jimbo hilo waliopo nchini kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya jukwaa la biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat 2019.
Jimbo la Gujarat lina pato la ndani la dola za Marekani bilioni 15 na linachangia asilimia 17 ya pato la viwanda nchini India na ni jimbo lenye viwanda vikubwa duniani.
Jimbo hilo pia linatoa mchango wa mauzo ya nje kwa asilimia 22 na asilimia 40 ya mizigo inayosafirishwa nchini india.
Akielezea Fursa za Uwekezaji zilizopo Gujarat katika semina maalum kwa wafanyabiashara wa Tanzania jijini Dar es salaam, Balozi wa India nchini Bw. Sandeep Arya amesema Watanzania wana fursa kubwa ya kushiriki uchumi wa Gujarat kwa kuona maeneo ya kushrikiana kiuchumi katika pande hizo mbili.
Akizungumza katika mkutano huo Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dk Reginald Mengi, ambaye ni Mwenyekiti mstaafu wa TPSF, aliwataka wawekezaji wa India kuja nchini kuwekeza kwa ubia na Watanzania, hususan katika maeneo ya utafiti, ubunifu na uongezaji thamani kwa mazao ya kilimo.
Aidha Mwenyekiti wa Shirikisho la wenye viwanda nchini CTI Bw. Shubhash Patel, Kaimu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo – TCCIA Bw.Octovian Mshiu walisema mkutano huo ni muhimu katika kuendeleza ushirikiano wa kibiashara baina ya Tanzania na India wenye historia ndefu.
Hayo yamezungumzwa katika mkutano mkubwa wa wafanyabiashara kutoka jimbo hilo waliopo nchini kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya jukwaa la biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat 2019.
Jimbo la Gujarat lina pato la ndani la dola za Marekani bilioni 15 na linachangia asilimia 17 ya pato la viwanda nchini India na ni jimbo lenye viwanda vikubwa duniani.
Jimbo hilo pia linatoa mchango wa mauzo ya nje kwa asilimia 22 na asilimia 40 ya mizigo inayosafirishwa nchini india.
Akielezea Fursa za Uwekezaji zilizopo Gujarat katika semina maalum kwa wafanyabiashara wa Tanzania jijini Dar es salaam, Balozi wa India nchini Bw. Sandeep Arya amesema Watanzania wana fursa kubwa ya kushiriki uchumi wa Gujarat kwa kuona maeneo ya kushrikiana kiuchumi katika pande hizo mbili.
Akizungumza katika mkutano huo Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dk Reginald Mengi, ambaye ni Mwenyekiti mstaafu wa TPSF, aliwataka wawekezaji wa India kuja nchini kuwekeza kwa ubia na Watanzania, hususan katika maeneo ya utafiti, ubunifu na uongezaji thamani kwa mazao ya kilimo.
Aidha Mwenyekiti wa Shirikisho la wenye viwanda nchini CTI Bw. Shubhash Patel, Kaimu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo – TCCIA Bw.Octovian Mshiu walisema mkutano huo ni muhimu katika kuendeleza ushirikiano wa kibiashara baina ya Tanzania na India wenye historia ndefu.
Katibu Mkuu (idara ya usambazaji maji) na Mwenyekiti wa GWSSB wa
Serikali ya Gujarat nchini India, J.P. Gupta akieleza fursa zilizopo
katika maeneo mbalimbali jimbo la Gujarat nchini India wakati wa mkutano
mkubwa wa wafanyabiashara kutoka Jimbo la Gujarat nchini India waliopo
nchini kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya
jukwaa la biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat
uliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti mstaafu wa TPSF ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa
Makampuni ya IPP Ltd, Dk Reginald Mengi akizungumza na wafanyabiashara
wa jimbo la Gujarat na Tanzania wakati wa mkutano mkubwa wa
wafanyabiashara kutoka Jimbo la Gujarat nchini India waliopo nchini kwa
ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya jukwaa la
biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat uliofanyika
katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Shirikisho la wenye viwanda nchini CTI Bw. Shubhash Patel
akizungumza na wageni waalikwa wakati wa mkutano mkubwa wa
wafanyabiashara kutoka Jimbo la Gujarat nchini India waliopo nchini kwa
ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya jukwaa la
biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat uliofanyika
katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
Pichani juu na chini ni sehemu ya Wafanyabishara kutoka Tanzania
walioshiriki mkutano mkubwa wa wafanyabiashara kutoka Jimbo la Gujarat
nchini India waliopo nchini kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji
ikiwa ni sehemu ya jukwaa la biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa
Biashara wa Gujarat uliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini
Dar es Salaam.
Sektretarieti iliyoandaa mkutano huo kutoka jimbo la Gujarat katika
picha ya pamoja na meza kuu mara baada ya kumalizika kwa mkutano mkubwa
wa wafanyabiashara kutoka Jimbo la Gujarat nchini India waliopo nchini
kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji ikiwa ni sehemu ya jukwaa la
biashara ndani ya Mkutano Mkubwa wa Biashara wa Gujarat 2019 uliofanyika
katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...