Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe ameuagiza Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Tabora kujiridhisha kwa kuyapima tena madaraja na makalavati yaliyoanza kutengenezwa kwenye ujenzi wa barabara ya Usesula-Komanga yenye urefu wa KM 108 kama yanakidhi ubora na viwango kwa kuwa mchanga uliotumika haufai.
Waziri Mhandisi Kamwelwe amesema kuwa hata eneo ambalo mkandarasi anasaga mawe kuna vumbi jingi kulinganisha na kokoto zinazozalishwa hii kitaalamu ina maanisha kwamba mwamba huo wa mawe ni dhaifu.
Ameyasema hayo katika kijiji cha Ipole wilayani Sikonge wakati akikagua ujenzi wa barabara hiyo na kusema kuwa hana imani na mhandisi mshauri kutoka kampuni ya LEA International Ltd katika usimamizi wa mradi huu.
"Sijaridhishwa na madaraja na makalvati haya Mhandisi wa Mkoa kushirikiana na Mhandisi Mshauri na Mkandarasi mkayapime tena ubora kwenye Maabara ya Taifa na kama hayafai muyaondoe maramoja na kutengeneza mengine",amesema Waziri Mhandisi Kamwelwe
Amesisitiza kuwa fedha za kujengea barabara hiyo zimefedhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na tutalazimika kuzilipa hivyo ni lazima thamani ya fedha inaonekana katika mradi huu.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe, akitoa
maelekezo kwa Mhandisi Mshauri kutoka Kampuni ya LEA International Bw.
Sanjeev Gupta (kushoto) anayesimamia ujenzi wa barabara ya
Usesula-Komanga yenye urefu wa KM 108 kwa kiwango cha lami, wakati
akikagua hatua za ujenzi wa barabara hiyo na kutoridhishwa na madaraja
na makalvati yaliyotengenezwa katika mradi huo, mkoani Tabora.
Fundi
Mchundo Bw. Fadhili Amiri, akitoa ufafanuzi kwa Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe, (wa pili kushoto)
kuhusu kazi anazozifanya wakati alipokuwa akikagua hatua za ujenzi wa
barabara ya Usesula-Komanga yenye urefu wa KM 108 kwa kiwango cha lami,
mkoani Tabora.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe, akikagua
mchanga unaotumika kutengenezea madaraja na makalvati katika ujenzi wa
barabara ya Usesula-Komanga yenye urefu wa KM 108 kwa kiwango cha lami,
na kutoridhishwa na ubora wake, mkoani Tabora.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe,
akizungumza na Mhandisi Mshauri kutoka Kampuni ya LEA International Bw.
Sanjeev Gupta anayesimamia ujenzi wa barabara ya Usesula-Komanga yenye
urefu wa KM 108 kwa kiwango cha lami, wakati akikagua kokoto
zitakazotumika katika mradi huo na kutoridhishwa nazo, mkoani Tabora.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe, (wa
kwanza) akisisitiza jambo kwa Mkandarasi wa Kampuni ya SAMOTA Bw.
Abdallah Salim, kuhusu kukamilisha mradi huo kwa wakati, mara baada ya
kukagua hatua za maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Urambo-Kaliua yenye
urefu wa KM 28, Mkoani Tabora.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...