Naibu Spika wa Bunge Mh. Dkt. Tulia Ackson
akimwakilisha Spika wa Bunge Mh. Job Ndungai aliongoza Harambee ya changizo la
fedha kwa ajili ya maendeleo chuo cha St. Mark’s ambacho kipo Buguruni Malapa
Jijini Dar es Salaam.
Katika harambee hiyo Dkt. Tulia aliwezesha
kuchangisha Tsh Milioni 284 kwa umahili mkubwa ambapo alitumia njia mbalimbali
pamoja na mistari ya Bibilia ambayo iliwahamasisha watu wengi
kuchangia jambo ambalo wengi hawakutarajia.
Katika harambee hiyo pamoja na waumini na wageni
mbalimbali kuhamasishwa kuchangia fedha hizo na
Dkt. Tulia, lakini pia bila woga aliwabana Maaskofu, wachungaji na
wainjilisti ili wapate kuchangia katika harambee hiyo.
Naibu Spika wa Bunge Mh. Dkt Tulia Ackson akizindua rasmi harambee ya kuchangia maendeleo ya chuo cha St. Mark's ambapo alisema kuwa yeye hato ongea mengi zaidi ya kukusanya fedha kwa kuwa jambo hilo ni muhimu.
Mgeni rasmi Naibu Spika wa Bunge Mh. Dkt Tulia Ackson(Kushoto) akipokea zawadi kutoka chuo cha St. Mark's.
Mgeni Rasmi Naibu Spika wa Bunge Mh. Dkt Tulia Ackson pamoja na Meza kuu wakitoa mkono wa salam wakati waumini na wageni waalikwa walipokuwa wakitoa sadaka.
Waumini, Waalikwa mbalimbali pamoja na watumishi wa Chuo cha St. Mark's wakiwa katika Harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya maboresho ya Chuo hicho.
Kwa ambao wangependa kuchangia wanaweza kutumia njia zifuatazo
TIGO PESA : 0677058716
CRDB BANK: 0150237155300 (HOLLAND BRANCH)
TIB : 004600000860601 (SAMORA DAR ES SALAAM)
(Picha zote na Fredy Njeje)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...