Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii
MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda jana amezindua ujenzi wa Ofisi moja Kati ya ofisi mbili za kisasa katika shule ya msingi Vijibweni katika Manispaa ya Kigamboni ikiwa ni ahadi alizoahidiwa na Kampuni ya Ujenzi ya CRJE iliyoguswa na Kampeni ya Makonda ya Ujenzi wa Ofisi 402 za walimu katika jiji la Dar es salaam.
Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika katika shule ya msingi Vijibweni ambako ni moja ya shule ambayo ofisi za walimu zitajengwa Makonda amesema kuwa moja kati ya vitu vinavyomnyima usingizi ni kuona walimu wanafanya kazi katika mazingira magumu ikiwemo kufanya kazi chini ya miti na kwenye korido na lengo la kuanzisha kampeni hiyo ni kuhakikisha thamani walimu inarejea.
Aidha Makonda amesema uwepo wa mazingira bora ya kufanyia kazi kwa walimu Ndio chachu ya kuongezeka kwa ufaulu ambapo amewapongeza walimu na watendaji wa elimu kwa kuifanya Dar es salaam kuongoza kitaifa katika matokeo ya mtihani wa Darasa la Saba.Pia Makonda amesema kuwa ofisi hizo zitakuwa na mahitaji yote muhimu ikiwemo ofisi ya mwalimu mkuu, mwalimu mkuu msaidizi, ukumbi wa mikutano, ofisi ya walimu wote, chumba cha mitihani, chumba cha mhasibu, mapokezi, stoo, Vyoo na Bafu.
Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Sarah Msafiri amesema kuwa kama watendaji wataendelea kuunga mkono jitihada za Mh. Rais na Mkuu wa Mkoa katika suala zima la elimu ili kuhakikisha watoto wanapata elimu iliyo bora na walimu wanafanya kazi zao katika mazingira ya kuridhisha.Diwani wa kata ya Vijibweni na Mstahiki Meya wa jiji la Dar es salaam Isaya Mwita amesema kuwa anashukuru kwa kufanya kazi na viongozi kwa ushirikiano bila kujali itikadi za vyama.
Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Vijibweni amemueleza Mkuu wa Mkoa kuwa shule hiyo haina ofisi yoyote ya walimu hivyo wamekuwa wakifanyia kazi chini ya miti na kwenye korido ambapo wamemshukuru kwa kuwaletea mfadhili wa kuwajengea ofisi ya kisasa.
RC Makonda akiwa ameongozana na baadhi ya viongozi wa maispaa ya Kigamboni akikagua madarasa ya wanafunzi wa Shule ya msingi ya vijibweni katika uzinduzi wa ujenzi wa ofisi za walimu ikiwa ni muendelezo wa ilani yake kujenga ofisi hizo 402 hapa Jijini Dar es Salaam.
RC Makonda akiwapungia wanafunzi mkono wa kwaheri Mara baada ya zoezi la uzinduzi wa ujenzi wa ofisi kumalizika jana Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akizungumza jana na wageni waaliohudhuria wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa ofisi mbili za kisasa za walimu wa Shule ya msingi ya vijibweni iliyopo katika manispaa ya Halmashauri ya Kigamboni Jijini Dar es Salaam akitimiza ahadi aliloahidiwa na kampuni ya ujenzi ya CRJE kutoka nchini China iliyoguswa na kampeni ya RC Makonda ya kujenga ofisi 402 za walimu.
MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda jana amezindua ujenzi wa Ofisi moja Kati ya ofisi mbili za kisasa katika shule ya msingi Vijibweni katika Manispaa ya Kigamboni ikiwa ni ahadi alizoahidiwa na Kampuni ya Ujenzi ya CRJE iliyoguswa na Kampeni ya Makonda ya Ujenzi wa Ofisi 402 za walimu katika jiji la Dar es salaam.
Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika katika shule ya msingi Vijibweni ambako ni moja ya shule ambayo ofisi za walimu zitajengwa Makonda amesema kuwa moja kati ya vitu vinavyomnyima usingizi ni kuona walimu wanafanya kazi katika mazingira magumu ikiwemo kufanya kazi chini ya miti na kwenye korido na lengo la kuanzisha kampeni hiyo ni kuhakikisha thamani walimu inarejea.
Aidha Makonda amesema uwepo wa mazingira bora ya kufanyia kazi kwa walimu Ndio chachu ya kuongezeka kwa ufaulu ambapo amewapongeza walimu na watendaji wa elimu kwa kuifanya Dar es salaam kuongoza kitaifa katika matokeo ya mtihani wa Darasa la Saba.Pia Makonda amesema kuwa ofisi hizo zitakuwa na mahitaji yote muhimu ikiwemo ofisi ya mwalimu mkuu, mwalimu mkuu msaidizi, ukumbi wa mikutano, ofisi ya walimu wote, chumba cha mitihani, chumba cha mhasibu, mapokezi, stoo, Vyoo na Bafu.
Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Sarah Msafiri amesema kuwa kama watendaji wataendelea kuunga mkono jitihada za Mh. Rais na Mkuu wa Mkoa katika suala zima la elimu ili kuhakikisha watoto wanapata elimu iliyo bora na walimu wanafanya kazi zao katika mazingira ya kuridhisha.Diwani wa kata ya Vijibweni na Mstahiki Meya wa jiji la Dar es salaam Isaya Mwita amesema kuwa anashukuru kwa kufanya kazi na viongozi kwa ushirikiano bila kujali itikadi za vyama.
Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Vijibweni amemueleza Mkuu wa Mkoa kuwa shule hiyo haina ofisi yoyote ya walimu hivyo wamekuwa wakifanyia kazi chini ya miti na kwenye korido ambapo wamemshukuru kwa kuwaletea mfadhili wa kuwajengea ofisi ya kisasa.

RC Makonda akiwa ameongozana na baadhi ya viongozi wa maispaa ya Kigamboni akikagua madarasa ya wanafunzi wa Shule ya msingi ya vijibweni katika uzinduzi wa ujenzi wa ofisi za walimu ikiwa ni muendelezo wa ilani yake kujenga ofisi hizo 402 hapa Jijini Dar es Salaam.

RC Makonda akiwapungia wanafunzi mkono wa kwaheri Mara baada ya zoezi la uzinduzi wa ujenzi wa ofisi kumalizika jana Jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akizungumza jana na wageni waaliohudhuria wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa ofisi mbili za kisasa za walimu wa Shule ya msingi ya vijibweni iliyopo katika manispaa ya Halmashauri ya Kigamboni Jijini Dar es Salaam akitimiza ahadi aliloahidiwa na kampuni ya ujenzi ya CRJE kutoka nchini China iliyoguswa na kampeni ya RC Makonda ya kujenga ofisi 402 za walimu.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...