Mwenyekiti
wa Makampuni ya Kiluwa Group Ltd,Mohamed Kiluwa ( wa nne kulia) pamoja
na ujumbe wake wakiwa na wageni wao katika picha ya pamoja kwenye moja
ya chumba maalum cha kufikia Wageni katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa
wa Julius Nyerere,mara baada ya kuwasili Oktoba 27,2018 jijini Dar
kutoka nchini China .Kampuni hiyo yenye ujumbe wa watu wa Watano umekuja
nchini kwa mwaliko wa kampuni ya Kiluwa Group Ltd kufanya mazungumzo
mbalimbali yakiwemo ya kutafuta fursa za uwekezaji ikiwemo pia kuonana
na uongozi wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC).
Mwenyekiti
wa Makampuni ya Kiluwa Group Ltd,Mohamed Kiluwa pamoja akipokea zawadi
aliyoletewa na mgeni wake,Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Yinengda
New Material Technology,Mayi
Hong mara kwenye moja ya chumba maalum cha kufikia Wageni katika uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,mara baada ya kuwasili Oktoba 27,2018 kutoka
nchini China.
Mwenyekiti
wa Makampuni ya Kiluwa Group Ltd,Mohamed Kiluwa pamoja na Mkurugenzi
Mtendaji wa kampuni ya Yinengda New Material Technology,Mayi
Hong wakimsikiliza Meneja wa kampuni ya Kiluwa Group Ndugu Madoweka
(ambaye ni mkalimani wa lugha ya Kichina),akifafanua jambo kurahisisha
mawasiliano kwa mgeni wao Ndugu Mayi Hong akiwa ameambatana na ujumbe
wake wa watu wanne kutoka kwenye kampuni yake ambayo inajishughulisha na
uzalishaji/utengenezaji wa bidhaa za
ngozi nchini China.
Mkurugenzi
wa Kampuni ya Kiluwa Group,Naima Kiluwa akisalimiana na Mkurugenzi
Mtendaji wa kampuni ya Yinengda New Material Technology,Mayi
Hong,mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa
Julius Nyerere,jijini Dar Oktoba 27,2018.
Mkurugenzi
wa Kampuni ya Kiluwa Group,Naima Kiluwa pichani kati akiwa ameambatana
na Wageni wake mara baada ya kuwapokea jana uwanja wa Ndege wa Kimataifa
wa Julius Nyerere wakitokea nchini Chaina,Pichani kulia ni Mkurugenzi
Mtendani wa kampuni ya Yinengda New Material Technology,Mayi
Hong.kampuni hiyo inajishughulisha na uzalishaji/utengenezaji wa bidhaa
za ngozi nchini China.







Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...