·
Mmoja anaswa na bastola,risasi 42 na magazine mbili, fedha
tasilimu sh. milioni 1.3 za hongo barabarani, simu tatu na kadi nane za
mitandao tofauti.
· Mwingine anaswa na Bendera ya Taifa, king’amuzi cha Startimes
NA BALTAZAR MASHAKA, MWANZA
MAJAMBAZI sugu wawili hatari wamenaswa na Jeshi la Polisi mkoani Mwanza waiwa na silaha na vitu mbalimbali baada ya kufanya uhalifu katika matukio mawili tofauti.
Majambazi hao Peter Thomas Nyanchiwa au Smart Boy mkazi wa jijini Dar Es Salaam, alikamatiwa eneo la Runzewe mkoani Geita huku Jackson Elias maarufu Longoko (20) mkazi wa Shamaliwa Igoma katika Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza akikamatwa Oktoba 3, majira ya saa 11:00 alfajiri akiwa nyumbani kwake.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza (RPC) Kamishna Msaidizi (ACP) Jonathan Shanna alisema majambazi hao walikuwa wakiwatesa wananchi kutokana na uhalifu wa kutumia silaha wakiwavunjia nyumba na kuwapora mali na fedha .
Alisema tukio la kwanza jambazi Peter akiwa na wenzake wawili walikodisha gari hilo jijini Mwanza kutoka kwa mmiliki wake kwenda kuwachukua watalii wakidai wameharibikiwa gari lao katika mbuga ya wanyama Serengeti ili kuwawezesha kuendelea na safari ya kutalii kwenye mbuga hiyo.
NA BALTAZAR MASHAKA, MWANZA
MAJAMBAZI sugu wawili hatari wamenaswa na Jeshi la Polisi mkoani Mwanza waiwa na silaha na vitu mbalimbali baada ya kufanya uhalifu katika matukio mawili tofauti.
Majambazi hao Peter Thomas Nyanchiwa au Smart Boy mkazi wa jijini Dar Es Salaam, alikamatiwa eneo la Runzewe mkoani Geita huku Jackson Elias maarufu Longoko (20) mkazi wa Shamaliwa Igoma katika Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza akikamatwa Oktoba 3, majira ya saa 11:00 alfajiri akiwa nyumbani kwake.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza (RPC) Kamishna Msaidizi (ACP) Jonathan Shanna alisema majambazi hao walikuwa wakiwatesa wananchi kutokana na uhalifu wa kutumia silaha wakiwavunjia nyumba na kuwapora mali na fedha .
Alisema tukio la kwanza jambazi Peter akiwa na wenzake wawili walikodisha gari hilo jijini Mwanza kutoka kwa mmiliki wake kwenda kuwachukua watalii wakidai wameharibikiwa gari lao katika mbuga ya wanyama Serengeti ili kuwawezesha kuendelea na safari ya kutalii kwenye mbuga hiyo.
Jambazi sugu Peter Thomas Nyanchiwa anayedaiwa kuiba gari na kumjeruhi dereva wa gari hilo kwa risasi akionyeshwa kwa waandishi wa habari na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza (RPC) ACP Jonathan Shanna (kushoto). Picha na Baltazar Mashaka.

Mtuhumiwa wa Ujambazi Jackson Elias akitambulishwa wkwa waandishi habari jana baada ya kutiwa mbaroni na polisi kuhusiana na tukio la uhalifu.Kushoto ni Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza (RPC) Kamishna Msaidizi wa polis (ACP) Jonathan Shanna. wengine ni maofisa na askari wa jeshi hilo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza (RPC) Jonathan Shanna akiwasomea waandishi wa habari majina ya hati ya kusafiria ya mtuhumiwa wa ujambazi Peter Thomas Nyachiwa.

Kamanda Jonathan Shanna akiwaonyesha wana habari gari T 122 DLY lilioibwa na majambazi kabla ya kukamatwa huko Runzewe mkoani Geita.
Mtuhumiwa wa Ujambazi Jackson Elias akitambulishwa wkwa waandishi habari jana baada ya kutiwa mbaroni na polisi kuhusiana na tukio la uhalifu.Kushoto ni Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza (RPC) Kamishna Msaidizi wa polis (ACP) Jonathan Shanna. wengine ni maofisa na askari wa jeshi hilo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza (RPC) Jonathan Shanna akiwasomea waandishi wa habari majina ya hati ya kusafiria ya mtuhumiwa wa ujambazi Peter Thomas Nyachiwa.
Kamanda Jonathan Shanna akiwaonyesha wana habari gari T 122 DLY lilioibwa na majambazi kabla ya kukamatwa huko Runzewe mkoani Geita.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...