Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii, Kanda ya Kaskazini.
JESHI la Polisi mkoa wa Kilimanjaro kwa kushirikiana na
Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) wamefanikiwa
kukamata kiwanda cha kutengeneza Pombe
kali ambacho kimekuwa kikizalisha bidhaa hiyo bila ya usajili.
Moja ya dira za serikali ya awamu ya tano ni kufikia uchumi
wa kati kupitia Viwanda ,hata hivyo baadhi ya wafanyabiahara watafsiri Dira hii
tofauti kwa kuamua kuanzisha Viwanda bila ya kufuata matakwa ya Sheria na
taratibu za nchi.
Hali hii imejidhihirisha mkoani Kilimanjaro katika mji mdogo
wa Himo baada ya Polisi,TRA na TFDA kubaini uwepo wa kiwanda bandia
kinachozalisha Pombe kali .
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro ,Kamishna Msaidizi wa
Polisi ,Hamisi Issah amesema jeshi la Polisi litaendelea kushirikiana na idara
nyingine za serikali kuhakikisha kodi ya serikali inapatikana pamoja na
kuhakiki ubora wa bidhaa kwa ajili ya afya ya watumiaji.
Zoezi la kubaini uwepo wa viwanda bandia katka mkoa wa
Kilimanjaro ambapo katika siku za karibuni viwanda vilivyogundulika ni vile
vinavyotengeneza Pombe za kienyeji na Pombe kali ,baadhi vikiwa katika wilaya ya Rombo.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro,Hamisi Issah akitizama baadhi ya chupa
ambazo zimendaliwa kwa ajili ya kujaza kimiminika cha Pombe kali.
Sehemu
ya Mitambo iliyopo ndani ya kiwanda hicho kilichopo katika wilaya ya
Himo ambacho kinaaminika kuhusika katika kutengeneza Pombe kali bila ya
kufuata taratibu.
Anayedaiwa
kuwa mmoja wa wafanyakazi wa kiwanda hicho akitoa maelezo kwa kamanda
wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro ,Hamisi Issah pamoja na Meneja Msaidizi wa
TRA Kilimanjaro anayeshughulikia masuala ya forodha ,Godfrey Kitundu
ndani ya kiwanda hicho.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...