Na Agness Francis, Blogu ya Jamii

MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amemuagiza mwanadada Amber Rutty anayejihusisha na masuala ya muziki wa bongo fleva nchini kufika katika kituo chochote cha Polisi hapa jijini leo  kabla ya saa 12 Jioni.

Rc Makonda kupitia ukurasa wake wa Instagram ameweka picha ya mwanadada huyo na kuandika haya :

"Wakati TCRA wakijipanga kuchukua hatua, mimi namtaka mwenye picha hii kufika kituo chochote cha Polisi kilichopo karibu na eneo lake kabla ya saa 12 jioni. Na ukifika waambie umeitwa na RC Makonda watakupatia ujumbe wako" ameandika  Makonda.

Hii inakuja baada kwa kosa la matumizi mabaya ya mtandao  linalomkabili kwa kusambaza Video ya  yenye maudhui ya kingono
na kusambaa kwenye mitandao ya kijamii na kuleta sintofahamu kubwa kwa Wanajaamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...