Mkuu wa Mkoa wa Mwanza , John Mongella  (katikati) akikabidhi zawadi ya cheti,medali na pesa taslimu kiasi cha sh mil. 4 kwa mwanariadha Mourice Masima Kutoka Kenya  aliemaliza katika nafasi ya kwanza kwenye mbio za km 42 Rock City Marathon zilizofanyika jijini Mwanza mwishoni  mwa wiki baada ya kutumia  muda wa saa 2:19:14.
 Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Kuhifadhi Mafuta ya TIPER, Bw Emmanuel Kondi akikabidhi  zawadi ya cheti,medali na pesa taslimu kiasi cha sh mil. 4 kwa mshindi wa kwanza mbio za km 42 kwa wanawake mwanariadha Naomi Jepngetich kutoka Kenya  aliyetumia muda wa saa 02:44:19 kukamilisha mbio hizo. Kulia  ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Bw John Mongella. TIPER ni moja ya wadhamini wakubwa wa mbio hizo.
 Mwakilishi kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Bi. Flora Ndutta akikabidhi  zawadi ya cheti,medali na pesa taslimu kiasi cha sh mil. 3 kwa mshindi wa kwanza mbio za km 21 mwanariadha Failuna Matanga kutoka Tanzania.
 Mwenyekiti wa Chama cha Riadha Mkoa wa Mwanza (MWAA) Bw Silas Lucas (kulia) akikabidhi zawadi  kwa mshindi wa kwanza mbio za KM 21 Emmanuel Giniki kutoka Tanzania alietumia saa 1:04:09 akifuatiwa na Mkenya Daniel Kayioki alietumia muda wa saa 1:04:47.
 Baadhi ya washiriki wa mbio za km 5 wakimalizia mbio hizo zilizohitimishwa kwenye viunga vya jengo la Rock City Marathon.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...