Mkuu wa Mkoa wa Mwanza , John Mongella (katikati) akikabidhi zawadi ya cheti,medali
na pesa taslimu kiasi cha sh mil. 4 kwa mwanariadha Mourice Masima Kutoka
Kenya aliemaliza katika nafasi ya kwanza
kwenye mbio za km 42 Rock City Marathon zilizofanyika jijini Mwanza
mwishoni mwa wiki baada ya kutumia muda wa saa 2:19:14.
Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Kuhifadhi Mafuta ya
TIPER, Bw Emmanuel Kondi akikabidhi zawadi ya cheti,medali na pesa taslimu kiasi
cha sh mil. 4 kwa mshindi wa kwanza mbio za km 42 kwa wanawake mwanariadha Naomi
Jepngetich kutoka Kenya aliyetumia muda
wa saa 02:44:19 kukamilisha mbio hizo. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Bw John Mongella.
TIPER ni moja ya wadhamini wakubwa wa mbio hizo.
Mwakilishi kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Bi.
Flora Ndutta akikabidhi zawadi ya
cheti,medali na pesa taslimu kiasi cha sh mil. 3 kwa mshindi wa kwanza mbio za
km 21 mwanariadha Failuna Matanga kutoka Tanzania.
Mwenyekiti wa Chama cha Riadha Mkoa wa Mwanza (MWAA)
Bw Silas Lucas (kulia) akikabidhi zawadi
kwa mshindi wa kwanza mbio za KM 21 Emmanuel Giniki kutoka Tanzania alietumia
saa 1:04:09 akifuatiwa na Mkenya Daniel Kayioki alietumia muda wa saa 1:04:47.
Baadhi ya washiriki wa mbio za km 5 wakimalizia mbio
hizo zilizohitimishwa kwenye viunga vya jengo la Rock City Marathon.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...