Kwa kipindi kirefu kumekuwepo na changamoto ya kimtazamo kati ya dhana ya Hifadhi ya Jamii na Fao la kujitoa, Changamoto hii kwa kiasi kikubwa inasababishwa na uelewa mdogo miongoni mwa wanachama na wadau wa sekta ya Hifadhi ya Jamii. Suala hili limepelekea malalamiko mengi huku wengine wakijutia kuchangia kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

Ili kulielewa jambo hili kwa mapana yake nianze kwa kuelezea dhana ya Hifadhi ya Jamii kama utaratibu unaowekwa na Jamii kwa lengo la kuwapatia wanajamii kinga dhidi ya majanga ya kiuchumi na kijamii yanayosababisha upungufu au upotevu wa kipato kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo ugonjwa, ukosefu wa ajira, ulemavu na uzee. Kuna aina mbili za mifumo ya hifadhi ya jamii ambayo ni mifumo rasmi na mifumo isiyo rasmi. Mifumo rasmi ni ile ambayo inawekwa kwa mujibu utaratibu, kanuni na Sheria zinazotungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mifumo isiyo rasmi ni ile ambayo jamii inajiwekea kupitia mila na desturi zake. 

Katika Mfumo rasmi wa Hifadhi ya Jamii umegawanyika katika makundi makubwa mawili ambayo ni Hifadhi ya Jamii kwa utaratibu misaada kwa jamii “Social Assistance Schemes” ambapo misaada na ruzuku hutolewa kwa jamii kuwapatia wananchi huduma za misingi za Hifadhi ya Jamii. Huduma hizo hutolewa kwa malengo mbalimbali kama vile; kugharamia elimu ya msingi, afya, maji, ruzuku, uzee, ulemavu na kukabiliana na majanga yanayotokea kwenye jamii. 

Pili ni Hifadhi ya Jamii katika utaratibu wa bima kwa jamii “social insurance”.  Aina hii ya hifadhi ya jamii ipo katika sehemu mbili ambazo ni sehemu ya kwanza ni Fao la jamii kwa mujibu wa Sheria; Wafanyakazi hupaswa kuchanga na kupata mafao kwa mujibu wa Sheria kama vile Mifuko ya pensheni na Fao la Afya. Sehemu ya pili ni Mfuko wa hiari “Supplementary Schemes”, ambapo Wanachama huchangia kwa hiari.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...