Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Eng. Evarist Ndikiro (katikati) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza siku ya kuanza kwa Maonesho ya Viwanda Mkoa wa Pwani ambayo yatafunguliwa rasmi tarehe 29 Oktoba 2018 na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, katika viwanja vya Saba Saba mjini Kibaha. Benki ya CRDB ni Mdhamini Mkuu wa Maonyesho hayo. Wengine pichani ni Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo (wa pili kulia), Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani, Theresia Mmbando (wa pili kushoto), Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa (kushoto) pamoja na Meneja wa Benki ya CRDB, Rosemary Nchimbi.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Eng. Evarist Ndikiro akimuonyosha kitu Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa (kushoto) wakati walipotembelea katika viwanja vya Saba Saba mjini Kibaha ambavyo vitatumika kwa Maonesho ya Viwanda Mkoa wa Pwani kuanzia tarehe 29 Oktoba 2018. Benki ya CRDB ni Mdhamini Mkuu wa Maonyesho hayo.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Eng. Evarist Ndikiro (wa pili kushoto) akielekeza jambo kwa mafundi wa JKT wanaoendelea na ujenzi katika viwanja vya Saba Saba mjini Kibaha ambavyo vitatumika kwa Maonesho ya Viwanda Mkoa wa Pwani kuanzia tarehe 29 Oktoba 2018.
Eneo la uwanja utakaotumika kwa Maonesho ya Viwanda Mkoa wa Pwani, likiwa katika hatua za maandalizi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...