Mkufunzi kutoka Baraza la Kilimo Tanzania Dkt Freddy Gamba akisisitiza jambo wakati akitoa mafunzo ya Uongozi na Utawala bora kwa wanachama wa Baraza la Kilimo Tanzania, ambapo wanachama hao wanatarajia kunufaika na mafunzo hayo kwa siku mbili yanayofanyika Dar es Salaam, huku lengo kuu ikiwa ni kuwajengea uwezo kiutendaji wanachama wa baraza katika taasisi wanazoziongoza. 
 Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Kilimo Tanzania Bi Janeth Bitegeko akisisitiza jambo kwa wanachama wa Baraza la Kilimo wanaoshiriki semina ya siku mbili ya Uongozi na Utawala bora, mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo zaidi wa kiutendaji wanachama wa Baraza la Kilimo Tanzania ambao ni viongozi katika taasisi wanazoziongoza.
 Baadhi ya wanachama wa Baraza la Kilimo Tanzania ambao wanatoka kwenye Taasisi za TAMPRODA, SECO,  SUWA Farmers Association, Agri link Tanzania na Morogoro Rural Agro Dealers  Association, wakifuatilia mafunzo ya Uongozi na Utawala bora, mafunzo hayo ya siku mbili yanayofanyika Dar es Salaam yameratibiwa na Baraza la Kilimo Tanzania.
 Mwenyekiti wa taasisi ya Morogoro Rural Agro Bw Michael Mpembwa akijadili jambo na washiriki wenzake na wa semina ya uongozi na uatawala bora, mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo wa kiutendaji wanachama wa baraza la kilimo Tanzania.
Afisa Uhamasishaji Maendeleo ya wanachama na Uhusiano Kimtandao kutoka Baraza la Kilimo Tanzania Bw Khalid Ngasa na washiriki wengine wa semina ya siku mbili ya Uongozi na Utawala Bora, Semina hiyo imelenga katika kuwajengea uwezo zaidi wa kiutendaji wa wanachama wa Baraza la Kilimo Tanzania ambao ni viongozi katika taasisi wanazoziongoza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...