Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Jerry Muro jana ameungana na wananchi wa kijiji cha LOSIKITO kata ya Mwandeti Halmashauri ya Arusha katika ujenzi wa shule Mpya ya sekondari ya losiko ambayo inajengwa Kwa nguvu za wananchi.
 
Dc Muro ameamua kuungana na wananchi katika kuhakikisha shule hiyo inaanza kutumika Mwaka 2019 Kwa lengo la kupunguza uhaba wa shule na vyumba vya madarasa Kutokana na ongezeko Kubwa la wananchi waliofaulu Elimu ya Msingi ambao wanapaswa kuingia Kidato Cha kwanza Mwaka 2019.Dc Muro anaendelea na ziara yake katika kata ya mwandeti iliyo halmashauri ya Wilaya ya ARUSHA
2
Dc Muro akiungana na Wananchi kushiriki ujenzi kuhakikisha shule hiyo inaanza kutumika Mwaka 2019 Kwa lengo la kupunguza uhaba wa shule na vyumba vya madarasa Kutokana na ongezeko Kubwa la wananchi waliofaulu Elimu ya Msingi ambao wanapaswa kuingia Kidato Cha kwanza Mwaka 2019.
index
Dc Muro akishiriki ujenzi wa shule  mpya ya sekondari ya Losiko katika kijiji ch Losiko,wilayani Arumeru,ikiwa ni sehemu ya muendelezo wa ziara yake iliyoanza jana katika kata ya mwandeti,katika halmashauri ya Wilaya ya Arusha ambapo Mkuu huyo wa Wilaya anatarajiwa kutembelea Kata zote 53 za Wilaya ya Arumeru.
1
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Jerry Muro akifafanua jambo mbele ya baadhi wa viongozi aliombatana nao alipokwenda kuungana na wananchi wa kijiji cha LOSIKITO kata ya Mwandeti Halmashauri ya Arusha katika ujenzi wa shule Mpya ya sekondari ya losiko ambayo inajengwa Kwa nguvu za wananchi.
3

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...