Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HELSB) imekutana na wanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu (DUCE) kwa ajili ya kutoa elimu kuhusiana na utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu.

Akizungumza na wanafunzi hao katika chuo hicho Meneja wa Upangaji Mikopo wa Bodi hiyo Julitha Miyedu amesema kuwa taratibu za kuomba mikopo ziko wazi na jinsi ya kuupata mkopo huo kutokana na vigezo na masharti vilivyoanishwa.Amesema kuwa Bodi ya Mikopo iko kwa ajili ya wanafunzi katika kuhakikisha kila mwenye vigezo vya mikopo anapata kwa wakati ili kuwezesha wanafunzi wasifikirie suala fedha katika kufanya mahitaji.

Miyedu elimu wanayoitoa kuhusiana na mikopo ni endelevu katika kuhakikisha kila mwanafunzi anapata uelewa wa bodi inavyochakata mikopo kwa wanafunzi.“Hatutamuacha mtu kwenye suala linalohusiana na utoaji mikopo nia ya bodi ni kuona kila mtu anapata mkopo kutokana vigezo vilivyoanishwa katika kuijenga nchi yetu na kupata watalaam mbalimbali”amesema Miyedu.

Nae Afisa Mawasiliano Mwandamizi wa Bodi ya Mikopo Veneranda Malima amesema kuwa wanafunzi wanatakiwa kusoma vitu katika mitandao na vipeperushi vya bodi kwa kupata taarifa kufika ofisi za bodi kwa vitu vikubwa.Amesema kuwa bodi imeweka mfumo wa Kielekroniki katika kurahisisha malipo ya mikopo kwa wanafunzi kupitia kwa maafisa wa mikopo wa chuo.

Malima amesema kuwa Bodi itaendelea kutoa taarifa katika utaratibu uliozoeleka hivyo wanafunzi wajiepushe na kupata taarifa katika sehemu zisizo rasmi.
 Meneja wa Upangaji Mikopo wa Bodi hiyo Julitha Miyedu akizungumza na wanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu (DUCE) kuhusiana na ujio bodi katika utoaji wa mikopo ya elimu juu , iliyofanyika katika ukumbi wa chuo hicho jijini Dar es Salaam.
  Afisa Mawasiliano Mwandamizi  wa Bodi ya  Mikopo ya Wanafunzi  wa Elimu ya Juu Veneranda Malima akizungumza na wanfunzi wa mwaka wa kwanza wa DUCE.
 Afisa Mikopo wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu (DUCE)   Salmon Daud akitoa maelezo kwa wanafunzi wa chuo hicho kuhusiana na utaratibu wa kupata mikopo ni mara baada ya kujiridhisha na taarifa.
 Baadhi ya Wanafunzi wa mwaka wa kwanza 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...