Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.

Kampuni ya TanzaRice International Ltd imesema kuwa mchele una fursa ya ajira kubwa lakini watu bado hawana uelewe ya kufanya biashara hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi wa kampuni hiyo Deo Mbasa amesema kuwa wamefanya utafiti na kuona biashara hiyo inaweza kuwakomboa wananchi kiuchumi kwa kuuza mchele huo kupitia kampuni.

Amesema kuwa wajasiriaali wakijiunga na kampuni hiyo wanaweza kupata mchele na kuuza kwa jamii inayowazunguka.Mbasa amesema kuna faida ya kuuza mchele kwani kinachotakiwa ni uaminifu wa mtu kwa kuchukua mchele bila ya kuwa na hela mara baada ya kujiunga na kampuni hiyo.

"Hatuwezi kila kitu tunafikiria mtaji wakati ukiwa na uaminifu unaweza kufanya biashara hata kama hauna mtaji na baadae ukawa umejikwamua kiuchumi"amesema Mbasa.
 Mkurugenzi wa TanzaRice Deo Mbasa akitoa maada wakati wa mafunzo ya wajasiriaali .
Mjasiriamali wa bidhaa ya Mchele kupitia kampuni hiyo Even John akizungumza mafanikio ya biashara ya mchele.
 Bidhaa ya mchele ikioneshwa kwa wajasiriamali katika mafunzo yaliyoandaliwa na kampuni ya TanzaRice
 washiriki wa wajasiriaali wa Mchele wakiwa katika mafunzo yaliyoandaliwa na kampuni ya TanzaRice
Mkurugenzi wa Kampuni ya TanzaRice Deo Mbasa akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na fursa iliyopo katika bidhaa ya mchele.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...