January Makamba amewataka wataalamu elekezi wa tathmini ya athari kwa mazingira kubadilika kiutendaji ili tasnia hiyo iendelee kukua na
kutoa mchango stahiki katika maendeleo ya taifa.
Akifungua Mkutano wa Pili wa Mwaka wa Chama cha Wataalamu Elekezi wa
Tathmini Athari kwa mazingira, ukaguzi na vibali vya awali jijijni
Dar es salaam mwishoni mwa wiki, Bw. Makamba alisema wataalamu elekezi wa mazingira wana umuhimu mkubwa katika ujenzi wa uchumi,lakini lazima wabadilike namna ya utendaji wao wa kazi.
‘’Katika changamoto za namna ya ufahamu na ufanywaji wa
tathimini na ukaguzi wa mazingira nyie kama chama mnauwezo wa
kujipanga kuanzisha programu za mafunzo na kubadilishana uzoefu (
Capacity Building) kwa kufanya hivo itasaidia kuboresha na kuimarisha
uwezo wenu wa kiutendaji,’’ alisema Waziri Makamba.
Waziri Makamba alisema suala la tathimini za athari kwa mazingira
linapewa kipaumbele ili kwenda sambamba na azma ya Serikali ya Awamu
ya Tano ya kujenga Uchumi wa Kati na Viwanda ifikapo mwaka 2025.
“Kuna changamoto kadhaa kwenye usajiri wa wataalam elekezi wa
mazingira kuhusu ulipwaji wa ada za mwaka ambapo serikali inapoteza
mapato yake. Taarifa ya NEMC inaonyesha kuwa mwaka 2018 wataalam
binafsi wanadaiwa jumla ya shilingi milioni 600, na makampuni
yanadaiwa jumla ya milioni 250 kama ada za mwaka,” alisema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...