Alex Sonna,Dodoma

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. Bashiru Ali, ametembele shamba linalomilikiwa na Kampuni ya Uhuru Media Group (UMG) inayosimamia magazeti ya Uhuru, Mzalendo na redio Uhuru, ikiwa ni mkakati wa kuanza uwekezaji wa ambapo kutajengwa mji wa kisasa pamoja na makao makuu ya ofisi za vyombo vya habari vya chama.

Dk. Bashiru aliambatana na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi, Msimamizi Mkuu wa Vyombo vya Habari vya Chama, Ernest Sungura pamoja na baadhi ya wataalam wa mipango miji.

Katibu mkuu alisisitiza umuhimu wa vyombo hivyo kuhamia Dodoma kuunga mkono uamuzi wa waasisi wa taifa pamoja na ule wa Rais Dk. John Magufuli, wa kuhamishia makao makuu ya nchi kwenye mkoa huo. "Nimekuja kuangalia eneo linalomilikiwa vyombo vya habari vya CCM kwa sababu sasa maeneo yanabadilika kuwa ya mipango miji. Tumekuja kuangalia usalama wa mipaka ili tuweze kupanga matumizi yake na vyombo vyetu viweze kuhamia Dodoma.

"Ni sehemu ya kuenzi mawazo na firka za viongozi, waasisi wa chama chetu na Baba wa taifa aliyeona mbali kwa kuichagua Dodoma kuwa Makao Makuu ya Chama na Serikali," Dk. Bashiru alisisitiza.Hata hivyo amesema kuwa tayari maombi ya kubadilisha matumizi ya eneo hilo kutoka shamba hadi kutumika kwa shughuli za kibiashara au viwanda, yameshafikishwa kwenye Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji ambaye ndie mwenye jukumu la kusimamia sheria kwani chama hakipaswi kuwa sehemu ya kuvunja sheria.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. Bashiru Ali (katikati) akiwa na Mkurugenzi wa jiji la Dodoma,Godwin Kunambi (kulia) alipotembelea shamba linalomilikiwa na Kampuni ya Uhuru Media Group (UMG) inayosimamia magazeti ya Uhuru, Mzalendo na redio Uhuru,ikiwa ni mkakati wa kuanza uwekezaji wa ambapo kutajengwa mji wa kisasa pamoja na makao makuu ya ofisi za vyombo vya habari vya chama.
Mlinzi wa shamba hilo Zebeayo Lemgoha (kushoto) akimueleza jambo Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. Bashiru Ali alipotembelea shamba linalomilikiwa na Kampuni ya Uhuru Media Group (UMG) inayosimamia magazeti ya Uhuru, Mzalendo na redio Uhuru,ikiwa ni mkakati wa kuanza uwekezaji wa ambapo kutajengwa mji wa kisasa pamoja na makao makuu ya ofisi za vyombo vya habari vya chama.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. Bashiru Ali ,akizungumza na Mlinzi wa shamba hilo Zebeayo Lemgoha (kushoto) ni Mkurugenzi wa jiji la Dodoma,Godwin Kunambi alipotembelea shamba linalomilikiwa na Kampuni ya Uhuru Media Group (UMG) inayosimamia magazeti ya Uhuru, Mzalendo na redio Uhuru,ikiwa ni mkakati wa kuanza uwekezaji wa ambapo kutajengwa mji wa kisasa pamoja na makao makuu ya ofisi za vyombo vya habari vya chama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...