Ni mara chache sana kwa vijana kuamua kuandika wimbo unaolenga kuelimisha jamii, mara nyingi sana tumekuwa tukisikia nyimbo za mapenzi au ku-bang na kujirusha lakini kwa namna ya kipekee kabisa kikundi cha Muziki cha Kiswahili na Sanaa (KINASA) wamekuja na wimbo unaoelimisha juu ya matumizi ya madawa ya Kulevya. 

Wimbo huo unaofahamika kama Narudi nyumbani ambao ndani yake umekuwa ukielezea kuwa mwathirika wa madawa sio muhalifu, anahitaji kusaidiwa na sio kutengwa, anahitaji kuheshimika na kuthaminika. Wimbo huo ulioandaliwa na Tanzania Bora Initiative chini za mzalishaji mahiri anyefanya vizuri kwenye game ya muziki (Mocco Geneius) na video kufanya na Adam Juma ambaye ni miongoni mwa ma-director wakubwa sana nchini Tanzania. 


Tembelea Katika link https://www.youtube.com/watch?v=5B7ru4V_mpQ kuona kile ambacho vijana wa kitanzania wanaweza kufanya kwa ajili na Vijana wenzao na nchi yao. Enjoy.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...