Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Rais wa Shirikisho la mpira wa kikapu Tanzania (TBF) Phares Magesa amesema kuwa Kocha wa Kikapu Matthew McCollister ataendesha mafunzo kwa vijana na kusaka vipaji.
Mafunzo hayo yatakayoendeshwa 7 Novemba yataanza saa 3 asubuhi na kutakuwa na ufunguzi wa mafunzo ya vijana ya kikapu, yatakayoendeshwa na Kocha huyo Matthew McCollister ambaye ni Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Marekani.
Mafunzo hayo yatafanyika viwanja vya JMK Youth Park, Dar es Salaam kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 11 jioni tarehe 7 na 8, Novemba, 2018.
Shirikisho la mpira wa kikapu Tanzania (TBF) linaomba vijana wote wanaopenda kushiriki katika mafunzo haya wafike JMK Park ili kufaidika na mafunzo hayo, ambapo pia Kocha huyo atachagua baadhi ya vijana wenye vipaji ambao watapatiwa nafasi ya kufanya mafunzo zaidi nchini Marekani.
Tayari Kocha huyo amefanya mafunzo kama haya Arusha tarehe 3 - 5 Novemba, 2018.
TBF inaishukuru Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya habari, utamaduni, sanaa na Michezo, Baraza la Michezo la Taifa (BMT), kituo cha michezo cha JMK Youth Park na wadau wengine kwa kufanikisha mafunzo na ziara hii Kocha Matthew.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...