NA TIGANYA VINCENT,RS TABORA.

UZALISHAJI na ubora wa tumbaku msimu ujao wa kilimo unaweza kushuka baada ya mbolea ya kukuzia zao hilo kuchewewa kuwafikia wakulima hadi hivi sasa.Kauli hiyo imetolewa jana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Adam Malunkwi kwa niaba ya Madiwani wenzake wakati wa kikao cha Baraza hilo.

Alisema hadi hivi sasa mbolea ya aina ya N.P.K bado hajifika kwa wakulima wakati msimu wa mvua umeshakaribia kuanza jambo linalotishia ubora na uzalishaji.Malunkwi alisema kitendo hicho sio tu kitamwathiri mkulima pekee pia mapato ya Halmashauri ya Urambo yataathirika kwa sababu sehemu kubwa inategemea tumbaku ili kupata mapato ya ndani kwa ajili ya shughuli mbalimbali za maendeleo.

Alisema kwa mujibu wa taarifa za Mzabuni ambayo amepewa jukumu la kusambaza mbolea kwa wakulima wa tumbaku, meli iliyobeba mbolea hiyo itawasili nchini tarehe 11 mwezi huu na inaweza kuchukua wiki mbili na kendelea kuwafikia wakulima jambo ambalo litafanya mazao ya wakulima yapitwe na wakati.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Magreth Nakainga akitioa ufafanuzi kwa Madiwani wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani kilichokuwa kikipitia taarifa utekelezaji kwa kila Kata wilayani humo jana.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Adam Malunkwi akifungua kikao cha Baraza la Madiwani cha kupitia taarifa za utekelezaji wa kila Kata wilayani Urambo jana.
Mbunge wa Jimbo la Urambo Magreth Sitta akichangia taarifa ya utekelezaji wa kila Kata wilayani Urambo wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Urambo jana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...