Mjadala Mkali wa kujadili Ripoti ya kamati ya fedha katika
Bunge la NNE la Afrika Mashariki,EALA umeendelea Jana huku wabunge
mbalimbali wakiendelea kumtupia lawama katibu Mkuu wa jumuiya ya Afrika
Mashariki EAC,Liberat Mfumukeko kuwa ndo chanzo cha ubadhidifu wa fedha
kiasi cha dola za Kimarekani Milioni 10 za jumuiya hiyo.
Katika kikao hicho
Mbunge wa Kenya Simoni Mbugua alitishia kujihudhulu nafasi yake ya
ubunge iwapo wahusika hawatachukuliwa hatua za kinidhamu.
“Katibu Mkuu kwa muda
mrefu amekuwa akifuja fedha na si pesa kidogo ukijumlisha fedha ambazo
zimepotea ni zaidi ya dola Milioni 10″Amesema.
Amesema fedha hizo
zinatoka kwa wachuuzi wa nchi wanachama ili zitumike kwa watu wa EAC
lakini zimekuwa zikipotelea Mifukoni mwa wachache bila sababu za msingi
“Fedha hizo zikitolewa
zinakuja zinaporwa na Katibu Mkuu na watu wake, wanapora na kuweka
kwenye mifuko yao ,Kwenye Masoksi wanabeba pesa zote ,sasa mwananchi
aliyeko kule anajua mambo yanaenda vizuri lakini sisi kama wabunge
tunasema inatosha ,hatutakubali tena” Amesema Mbugua
Aidha alisema kuwa yeye kama Mbunge afadhali atoke kwenye nafasi yake kuliko kuona jumuiya ikiharibiwa kwa kiasi hicho.
Aliongeza kuwa kulitaka
Bunge hilo kuiga utendaji wa Rais John Magufuli na Rais Kenyatta wa
Kenya ambao wameonyesha uwezo mkubwa wa kupambana na ufisadi kwa
kuwafunga watuhumiwa wanaopatika na hatia.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...