Mjadala Mkali wa kujadili Ripoti ya kamati ya fedha katika Bunge la NNE la Afrika Mashariki,EALA umeendelea Jana huku wabunge mbalimbali wakiendelea kumtupia lawama katibu Mkuu wa jumuiya ya Afrika Mashariki EAC,Liberat Mfumukeko kuwa ndo chanzo cha ubadhidifu wa fedha kiasi cha dola za Kimarekani Milioni 10 za jumuiya hiyo.
Katika kikao hicho Mbunge wa Kenya Simoni Mbugua alitishia kujihudhulu nafasi yake ya ubunge iwapo wahusika hawatachukuliwa hatua za kinidhamu.
“Katibu Mkuu kwa muda mrefu amekuwa akifuja fedha na si pesa kidogo ukijumlisha fedha ambazo zimepotea ni zaidi ya dola Milioni 10″Amesema.
Amesema fedha hizo zinatoka kwa wachuuzi wa nchi wanachama ili zitumike kwa watu wa EAC lakini zimekuwa zikipotelea Mifukoni mwa wachache bila sababu za msingi
“Fedha hizo zikitolewa zinakuja zinaporwa na Katibu Mkuu na watu wake, wanapora na kuweka kwenye mifuko yao  ,Kwenye Masoksi wanabeba pesa zote ,sasa mwananchi aliyeko kule anajua mambo yanaenda vizuri lakini sisi kama wabunge tunasema inatosha ,hatutakubali tena” Amesema Mbugua
Aidha alisema kuwa yeye kama Mbunge  afadhali atoke kwenye nafasi yake kuliko kuona jumuiya ikiharibiwa kwa kiasi hicho.
Aliongeza kuwa kulitaka Bunge hilo kuiga utendaji wa Rais  John Magufuli na Rais Kenyatta wa Kenya ambao wameonyesha uwezo mkubwa wa kupambana na ufisadi  kwa kuwafunga watuhumiwa wanaopatika na hatia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...