Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu
Hassan akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Tamasha la Mvinyo
lililofanyika kwenye uwanja wa Mashujaa jijini Dodoma. (Picha na Ofisi
ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suuhu
Hassan akimkabidhi zawadi ya picha Balozi wa Italia nchini Mhe.
Roberto Mengoni kwa mchango wa nchi yake katika kusaidia kilimo cha zabibu wakati wa uzinduzi wa Tamasha la Mvinyo kwenye
viwanja vya Mashujaa jijini Dodoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suuhu Hassan akimkabidhi cheti cha kutambua mchango wake katika sekta ya mvinyo na zao la zabibu Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Alkovintages Bw. Archard Kato wakati wa uzinduzi wa Tamasha la Mvinyo kwenye viwanja vya Mashujaa jijini Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu; Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Anthony Peter Mavunde akizungumza na Waziri Wakuu wa Staafu Mhe. Peter Mizengo Pinda (katikati) na John Samuel Malecela (kulia) wakati wa halfa ya uzinduzi wa Tamasha la Mvinyo lililofanyika kwenye viwanja vya Mashujaa jijini Dodoma
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suuhu Hassan akipata maelezo ya umuhimu wa zabibu ya Dodoma katika uzalishaji mvinyo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Alkovintages Bw. Archard Kato (kulia) wakati wa hafla ya uzinduzi wa tamasha la mvinyo Dodoma.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...