Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa leo Novemba 3, 2018, amefunga wiki ya maonesho ya viwanda Kibaha, Mkoani POwani, yaliyokuwa yakifanyika kwenye viwanja vya CCM-Sabasaba, eneo la Picha ya Ndege.

Moanesho hayo yaliyofunguliwa na Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan, Oktoba 29, 2018, yalilenga kuwakutanisha wazalishaji bidhaa za wviwanda na wanunuzi (masoko), ambapo pia taasisi za serikali zinazohusika na utoaji huduma mbalimbali zilishiriki pia.

Miongoni mwa taasisi hizo, ni Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi WCF, ambao kazi yake kubwa ni kutoa Fidia kwa wafanyaklazi walioumia, kuugua au kufariki kutokana na kazi.Moja ya ujumbe mkubwa alioutoa siku anafungua maonesho hayo kwa waajiri kote nchini, Makamu wa Rais aliuagiza

uongozi wa (WCF), kuendelea kuwafuatilia waajiri ambao bado hawajajisajili ili waweze kufanya hivyo.Makamu wa Rais alitoa wito huo leo Oktoba 29, 2018 alipotembelea banda la Mfuko huo kwenye maonesho ya viwanda Mkoa wa Pwani kwenye viwanja vya CCM-Sabasaba, Picha ya Ndege Mkoani humo.

Alisema viwanda vimeongezeka nchini na kwamba huduma za WCF zitahitajika sana kwa wakati huu na hivyo kuutaka uongozi wa Mfuko, kuhakikisha unaendelea na ufuatiliaji kwa waajiri wa zamani na wapya ambao bado hawajajisajili na kuwasilisha michango kwenye Mfuko watekeleze takwa hilo la kisheria ili mfanyakazi anapoumia aweze kupata haki yake ya fidia.
Mkurugenzi wa Uendeshaji, Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bw. Anselim Peter, (kushoto), akitoa elimu kuhusu kazi za Mfuko huo kwa baadhi ya watumishi wa umma na binafsi waliotembelea banda la Mfuko huo kwenye maonesho hayo leo Bovemba 3, 2018 
Mkurugenzi wa Uendeshaji, Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bw. Anselim Peter(kulia), akimsikilzia mwananchi huyo aliyetembelea banda la Mfuko aliyetaka kujua kazi za Mfuko huo.  
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, (kushoto), akimkabidhi cheti cha shukrani Kaimu Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Bw. Semu Mwakyanjala mwishoni mwa maonesho hayo leo Novemba 3, 2018. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimsikiliza Bibi Florence Max Mambali wakati alipotembelea banda la Kampuni ya kufuga kuku na kuzalisha vifaranga vya kuku ya Mkuza Chicks katika Maonesho ya Viwanda Mkoa wa Pwani yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Sabasaba uliopo katika eneo la Picha ya Ndege, Kibaha, Oktoba 3, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, Mawaziri na viongozi wengine wa juu serikalini, wakiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi na wawakilishi wa taasisi za umma na binafsi waliowezesha kufanyika kwa maonesho hayo. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...