KATIKA  hali  isiyoya kawaida   kikao  cha  baraza la madiwani  wa  Halmashauri ya  Manispaa ya  Iringa ambacho  kwa wiki  iliyopita  madiwani  wa chama  cha mapinduzi (CCM)  walisusia  kikao   hicho  mstahiki  meya   Alex  Kimbe amewashangaza  wengi  baada ya  kuendesha  kikao  kwa  dakika 32  na  kugoma kusikiliza  hoja binafsi .

Kikao   hicho  kilianza  saa 2.00  hadi saa 2.32  huku  madiwani  takribani 10 wa  chama  cha  demokrasia na maendeleo (Chadema)  wakiwa na ukumbini na CCM   akiwemo  diwani  mmoja pekee  na   naibu  meya  Joseph  Lyata    kiliweza  kuendeshwa  kwa aina  yake  baada ya  mstahiki  meya   kufungua  kikao  hicho  kwa   sala  baada ya hapo kuwaita  bila  kutokea wajumbe  watatu wawili wa CCM na mmoja wa  Chadema  kuuliza maswali ya  papo kwa  papo kwa  meya   .

Kutokana na  wajumbe hao  wa  kikao  kutokuwepo  alifunga  zoezi hilo  na  kuendelea  na agenda  nyingine za  kikao  ikiwa  ni pamoja na  kusoma  taarifa  za  kamati  mbali mbali  na  kuruhusu  wenye  maswali  juu ya kamati hizo  kuuliza maswali  baada ya  hapo  alitangaza  kuzikataa  hoja  binafsi  ambazo   takribani  tatu ambazo  zilikuwepo  kwa madai ya  kutozingatia  kanuni  za  baraza  hilo kwa  hoja  hizo  kufikishwa kwa maandishi kabla ya   kuletwa katika  baraza .

"  Ndugu  wajumbe  kwa  kuwa hakuna  hoja binasi  zilizopo  ni za mdomo  tuu  naomba  kumkaribisha katibu  wa  kikao kwa  maneno  machache na  baada ya  hapo  nifunge  kikao  chetu "  alisema  meya  Kimbe  .

Kuwa  anawashukuru  wajumbe  waliofika kwa  wakati katika  kikao  hicho  ambacho  kimsingi  kilitangazwa  kuanza saa 2 .00 asubuhi   hivyo  wajumbe  waliochelewa  wamechelewa  kikao   hicho  alisema  na  kutangaza  kufunga  kikao  huku  baadhi ya  madiwani  wakiendelea  kuwasili  ukumbini .

Wakizungumza mara  baada ya  kikao  hicho aliyekuwa  meya wa Manispaa ya  Iringa Aman Mwamwindi (CCM)  alisema anashangazwa na hatua ya  kikao  kumalizika kwa  muda  mufupi  wakati  kulikuwa na hoja za  msingi  hasa  kwenye kamati ya mazingira  juu ya  eneo la Kihesa  Kilolo  eneo la  uwekezaji  ambalo waziri  wa  ardhi nyumba na maendeleo ya makazi na  waziri wa TAMISEMI  walishauri  eneo hilo  kutojengwa  viwanja  vya   michezo na badala  yake  kujenga vitega uchumi kama  ukumbi wa  mikutano wa AICC .

lla alisema anashangazwa  kuona anapingwa na meya  na  kuwa   hoja   hiyo  haina nafasi katika  kikao  hicho  na  badala yake  kuzuia  kujadiliwa na  kukimbilia  kufunga  kikao .
Baadhi ya madiwani  Halmashauri ya  Iringa  wakiwa katika  baraza leo

KUSOMA ZAIDI  BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...