Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt.
Augustine Mahiga (kushoto) akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki
ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (katikati) wakati akimkaribisha ofisini
kwake, Jengo la LAPF, Jijini Dodoma leo. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya
Benki ya CRDB, Ally Laay. Viongozi wa Benki ya CRDB wapo jijini Dodoma
kwa lengo la kukutana na viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na
wateja wa Benki hiyo, sambamba na kumtambulisha Mkurugenzi Mtendaji wao
mpya ayepokea kijiti kutoka kwa Mtangulizi wake Dkt. Charles Kimei
ambaye amestaafu. Wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na
Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa.
Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt.
Augustine Mahiga (katikati) akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya
CRDB, Abdulmajid Nsekela (wa pili kushoto) alipokuwa akizungumzia
mikakati mbalimbali ya Benki hiyo pamoja na kujitambulisha kwake, baada
ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo. Wengine pichani ni
Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya CRDB, Ally Laay (wa pili kulia),
Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB,
Tully Mwambapa (kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Tawi la Benki ya CRDB
Dodoma, Rehema Hamisi.
Katibu
Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi),
Alhaj Eng. Mussa Iyombe (katikati) akikabidhi cheti cha shukrani kwa
Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya CRDB, Ally Laay pamoja na Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya
CRDB, Abdulmajid Nsekela, kwa mchango waliotoa kwa Kitengo cha Ukaguzi
na Ufuatiliaji Fedha cha TAMISEMI, wakati uongozi wa Benki hiyo
ulipomtembelea Katibu Mkuu huyo ofisini kwake, Jijini Dodoma leo. Kulia
ni Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB,
Tully Mwambapa na kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Ukaguzi na
Ufuatiliaji Fedha cha TAMISEMI, Miriam Mbaga.
Katibu
Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi),
Alhaj Eng. Mussa Iyombe (kushoto) akifafanua jambo mbele ya Mwenyekiti
wa Bodi ya Benki ya CRDB, Ally Laay pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa
Benki ya
CRDB, Abdulmajid Nsekela, wakati wa kikao chao kilichofanyika ofisini
kwake, jijini Dodoma leo.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro (katikati) akimsikiliza
Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya CRDB, Ally Laay (wa pili kulia) alipokuwa
akifafanua jambo wakati wa kumtambulisha Mkurugenzi Mtendaji wa Benki
ya
CRDB, Abdulmajid Nsekela aliyeteuliwa hivi karibuni kushika wadhifa
huo.
Katibu
Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean
Ndumbaro (katikati) akizungumza jambo wakati wa kikao chake na viongozi
wa Benki ya CRDB, waliofika ofisini kwake leo jijini Dodoma kwa lengo la
kumtambulisha Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya
CRDB, Abdulmajid Nsekela aliyeteuliwa hivi karibuni kushika wadhifa huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...